dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, June 4, 2013

Mbunge amwaga machozi Bungeni

NA SHARON SAUWA

4th June 2013


Mbunge wa Kondoa Kaskazini, Zabein Mhita (CCM)
Mbunge wa Kondoa Kaskazini, Zabein Mhita (CCM), amedondosha machozi bungeni baada ya kukumbuka jinsi alivyolazimika kupanda kwenye mti ili kupokea simu ya msiba wa mwanae.

Mhita ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Sayansi na Teknolojia na Elimu ya Juu, katika Serikali ya Awamu ya Tatu iliyoongozwa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, alimwaga machozi jana wakati akichangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka 2013/2014.

Alisema akiwa katika ziara zake katika kata ya Bereko kwenye jimbo lake 2005, aliambiwa kuwa anatafutwa nyumbani kwake.

“Wenyeji wa pale wakaniambia twende upande juu ya mti utapata mawasiliano, nikaenda na kupanda na nikaarifiwa kuwa mwanangu Najima amefariki,” alisema.

“Nakutaja mwanangu Najima huko uliko peponi kwenye kheri, mheshimiwa Naibu Spika nilipata simu ya msiba wa mwanangu nikiwa juu ya mti” alisema kwa majonzi. 

Hali hiyo ilimfanya kudondosha machozi na kutoa miwani yake kabla ya kuendelea kuongea kuwa tangu mwaka 2005 hadi leo hakuna mawasiliano katika maeneo hayo, jambo linawafanya wakazi wake kupanda kwenye miti ili kupata mawasiliano.

“Namkumbuka mtoto wangu hata leo nikienda Kondoa mahali pale maana hadi leo hakuna mawasiliano,”alisema Mhita ambaye pia aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii katika Serikali ya Awamu ya Nne.

Huku akisisitiza haiungi mkono bajeti hiyo, Mhita,  alisema wananchi wa Kondoa Kusini wamedhalilika kwa muda mrefu na akaitaka serikali kupeleka mawasiliano katika Jimbo la Kondoa Kaskazini.

Baada ya kumaliza kuchangia wabunge wa viti maalum, Suzan Kiwanga (Chadema) na Kuruthumu Mchuchuri (CUF), walimfuata na kumfariji.

Akijibu hoja hiyo, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa, alisema amesikitishwa na jambo hilo na kuahidi kuwa atalishughulikia tatizo hilo la mawasiliano haraka.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment