dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, April 10, 2016

MAALIM SEIF AKIJIBU MASWALI YA WAANDISHI ZANZIBAR 10/04/2016



Nataka
niweke wazi leo kwamba tulipofanya uamuzi wa kuususia uchaguzi haramu na batili wa tarehe 20 Machi, 2016 tuliamua kusimama juu ya uamuzi unaoheshimu misingi ya kikatiba ambayo watu wa Zanzibar tumeamua ndiyo inapaswa iongoze na iendeshe nchi yetu. Tulijua kwamba uamuzi huo utakuwa na athari kwa CUF na kwa Zanzibar lakini tulijua na tuliamini pia kwamba athari hiyo haiwezi kuwa kubwa zaidi kuliko gharama ya kuikanyaga Katiba na Sheria za nchi yetu na gharama za kupiga teke demokrasia, haki za binadamu na utawala wa sheria.

Tulipima na tukatafakari kwa kina na kuona ni kheri kumeza machungu ya athari binafsi kwetu lakini tusimame kidete na kifua mbele katika kutetea maamuzi ya watu wa Zanzibar waliyoyafanya tarehe 25 Oktoba, 2015, na pia kulinda misingi ya Katiba na Sheria za nchi yetu na misingi ya demokrasia na haki za watu. Tuliona hayo ni kheri kwa huko twendako badala ya kushiriki katika haramu ya ubakaji wa demokrasia na matumizi ya nguvu za kijeshi kulazimisha watawala wasio na ridhaa ya watu. Tulifanya maamuzi yale pia kwa lengo la kuepusha shari katika nchi yetu.

Leo Wazanzibari na dunia nzima ni mashahidi kwamba uamuzi ule ulikuwa sahihi na wa busara. Maana mateso na vitisho walivyokumbana navyo Wazanzibari wakati tumewaachia uchaguzi ule watawala waovu peke yao vilikuwa vya kiasi kile kilichoshuhudiwa. Je, tungeliamua kushiriki na kusimama kulinda na kutetea ushindi wetu hali ingekuwaje? Bila shaka nchi ingetumbukia katika machafuko ambayo watawala waovu walikuwa tayari yatokee kuliko kuridhia maamuzi halali ya wananchi wa Zanzibar.

Maamuzi yale yamethibitika pia kwamba ni sahihi kwa jinsi watu wa Zanzibar walivyoudharau na kuupuuza uchaguzi haramu na batili wa tarehe 20 Machi, 2016. Watawala waovu wa CCM waliwadharau watu wa Zanzibar na watu wa Zanzibar wakaamua kuwadharau wao tarehe 20 Machi 2016.

Kwa upande mwengine, uamuzi tuliouchukua na kuusimamia pia ni uamuzi uliosimama juu ya misingi ya heshima na misingi ya utu wa watu, ambayo yalikuwa ndiyo malengo sahihi ya Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, Hayati Mzee Abeid Amani Karume, malengo sahihi ya Chama cha Afro Shirazi na malengo sahihi ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964.

Kwa hakika, uamuzi wa kuupuuza na kuudharau uchafuzi wa tarehe 20 Machi, 2016 ni ushindi mwengine wa Zanzibar katika historia yake ya kisiasa.

No comments :

Post a Comment