dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, April 11, 2016

Mlima Kilimanjaro waipaisha Tanzania kimataifa


By Julius Mathias, Mwananchi
Dar es Salaam. Mlima Kilimanjaro umeendelea kuipaisha Tanzania kimataifa baada ya kushinda kivutio cha asili Afrika kwenye Tuzo za Utalii duniani (WTA) zilizofanyika juzi visiwani Zanzibar.
Mlima huo ni moja ya vipengele sita ambavyo Tanzania ilishinda baada ya kugombea vipengele ishirini kati ya zaidi ya 1,200 vilivyokuwa vinashindaniwa na nchi za Afrika na Bara Hindi.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Rais wa WTA, Graham Cooke aliwapongeza washindi wa tuzo hizo na kuwataka kujenga mtandao utakaokuza utalii kwa nchi pamoja na wadau mbalimbali wa sekta hiyo.
Wakati mlima huo ukishinda kipengele cha kivutio bora Afrika, tuzo nyingine zilienda kwa Four Seasons Safari Lodge Serengeti ikiwa ni hoteli bora ya mbugani, Beyond Mnemba Island Lodge ya Zanzibar iliyoibuka hoteli bora ya kisiwani.
Nyingine ni Singita Sasakwa Lodge iliyoshinda kuwa hoteli ya kifahari Afrika na hoteli yalipofanyika maonyesho hayo, Diamonds La Gemma dell’Est ikiwa ni hoteli bora ya ufukweni. Fastjet imeibuka kuwa ndege yenye gharama za chini zaidi Afrika.
Meneja Mkuu wa Diamonds La Gemma dell’Est, Andrew Cook aliishukuru WTA kwa kuipa heshima ya pekee Tanzania kuandaa na kusimamia tuzo hizo na kuichagua hoteli yake kati ya nyingi zilizopo nchini.
Washindi wengine wa jumla walikuwa Hoteli ya Serena iliyoibuka kidedea kwa hoteli bora Afrika wakati Shirika la Ndege la Kenya likiwa kinara wa huduma za usafiri na Shirika la Ndege la Seychelles likiongoza kwa Bara Hindi.

No comments :

Post a Comment