dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, April 12, 2016

Muwsa akakutana na nguvu ya umma

  • WANANCHI waliodai wamechoshwa na kuchukizwa na vitisho vya mlinzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Moshi (Muwsa), wamempora silaha aina ya short gun na kuisalimisha katika kituo kikuu cha Polisi Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro. Mlinzi aliyeporwa bunduki ni Steven James (52).











Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Kamishna Msaidizi Wilbroad Mtafungwa, alithibitisha jana kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa watu watatu wamekamatwa na polisi kuhusu na kumnyang’anya silaha hiyo.

Alisemja waliokamatwa baada ya kutokea kwa tukio hilo saa 8:00 mchana juzi Jumamosi ni Deogratius Munishi, Getruda Baltazari na Haiyusi Sabini maarufu kama Lyatonga, wote wakazi wa Shirimatunda.

Wananchi hao wanadaiwa kuwa, bila ya kujua walichokifanya kilikuwa kinaweka rehani, hali ya amani na usalama wa eneo hilo, walimnyang’anya silaha hiyo, baada ya kuivua singoni na kuishika mkononi, akiwatisha wananchi hao waondoke katika eneo la ujenzi wa chanzo cha maji cha Mkashilingi wilayani Hai.Uporaji huo ulifanyika, wakati mlinzi huyo alipofika kwenye lindo muda mfupi baada ya wananchi zaidi ya 200 kutembea kwa miguu, kilomita mbili na nusu kutoka Shirimatunda hadi Mkashilingi, kwa ajili ya kujionea ujenzi wa mradi wa majisafi na salama unavyoendelea.

Wakati wakiendelea na majadiliano, ghafla mwananchi mmoja alimsogelea mlinzi huyo na kumpora silaha kisha wengine wakaanza kushangilia na kuondoka eneo hilo, huku mlinzi huyo aliyekuwa amefuatana na bosi wake wa doria, wakilazimika kukimbia kwa kutumia pikipiki kujiokoa.

Baada ya tukio hilo, mmoja wa wananchi hao ambaye jina lake halikufahamika mara moja, aliishika bunduki hiyo mkononi, na kufuatwa na kundi kubwa la wananchi waliokuwa wakielekea Polisi Bomang’ombe kwa ajili ya kuikabidhi kwa Jeshi la Polisi.

Wananchi hao walikuwa wakipinga mchakato wa ujenzi wa mradi wa maji wa mkashilingi unaotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (Muwsa). Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Watumia Maji wa Shirimatunda, Cornel Mushi ni kwamba wananchi hao hawakubaliani na ujenzi huo kuendelea kutekelezwa bila ya kuwashirikisha, kwa kuwa wana haki zote kutokana na kumiliki hati halali za watumia maji.

No comments :

Post a Comment