Dar es Salaam. Huenda changamoto katika kilimo zikapata mwarobaini baada ya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kubuni miwani maalumu kwa ajili ya kugundua magonjwa na wadudu wanaoshambulia mimea shambani.
Leo, Mchumi wa Kilimo wa Kilimo kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine, Dk Anna Temu alisema miwani hiyo itawawezesha wakulima kuona wadudu na magonjwa yanayoshambulia mimea katika hatua za mwanzo.
Alisema miwani hiyo inayotambulika kitaalamu kama 'Agro Spectacles' itasaidia kuondoa tatizo linalowakabili wakulima wa Tanzania la kufahamu uharibifu wa mazao unapokuwa umekomaa iwapo tu fedha za kukamilisha wazo hilo zitapatikana.
“Miwani hii inaweza kuhakikisha ongezeko la mavuno ya mazao na hivyo kuboresha usalama wa chakula kwa nchi na mapato ya jumla kwa wakulima, ”alisema Dk Temu.
Akizungumzia changamoto ya kifedha, Dk Temu alisema inakwamisha miradi mingi ya tafiti ikiwamo masuala ya kilimo.
Akizungumza katika warsha hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Sayansi na Teknolojia, (Costech) DkHassan Mshinda aliwaomba wafadhili na Serikali kuongeza fedha za kufanyia tafiti ili kusaidia masuala mbalimbali ya maendeleo ikiwamo ya kilimo, biashara.
No comments :
Post a Comment