dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, April 15, 2016

WAFANYABIASHARA KUTOKA NCHINI OMAN WAFANYA ZIARA MKOANI TANGA

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maabara za Vetenari Tanzania "TVLA" Dkt. Furaha Mramba akiwakaribisha baadhi ya wafanyabiashara kutoka nchini Oman waliopo nchini kwa ziara ya siku tatu (3) inayomalizika leo, ambao walitembelea katika Taasisi ya utafiti na uchunguzi wa wadudu na magonjwa waenezayo "VVBDRI -TANGA" inayosimamiwa na wakala hiyo na kutembelea sekta ya mifugo ili kuweza kujionea fursa za uwekezaji kupitia miradi hiyo.

Kiongozi wa ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Oman Bw. Warith Al- Kharusi akieleza malengo ya ziara yao Mkoani Tanga ambapo alieleza kuwa wamekuja kutembelea mradi wa shamba la mifugo ili waweze kujionea fursa za uwekezaji zinazoweza kupatikana kupitia mradi huo na miradi mingine watakayoitembelea. 

Ujumbe wa wafanyabiashara kutoka Omani wakiongozwa na viongozi wakuu na maafisa wa Taasisi za TVLA na VVBDRI-TANGA wakiwasili katika shamba la utafiti Mivumoni lililopo Wilayani Pangani Mkoani Tanga lenye ukubwa wa ekari 12789.6 ili kuweza kuona shughuli za ufugaji zinazofanyika katika shamba hilo

Bw. Warith Al - Kharusi akijadili jambo na wafanyabiashara wenzie wakati walipokuwa wakitembelea shamba hilo linalofuga Ngo'mbe, mbuzi na Kondoo, ambapo mpaka sasa Taasisi ya VVBDRI - Tanga imeweza kutumia asilimia 20 ya shamba hilo kwaajili ya shughuli za ufugaji na sehemu inayobaki bado haitumiki.

No comments :

Post a Comment