Mike Wanjala alipelekwa kwa mganga baada ya jogoo kuwika kutoka
tumboni mwake. Picha: TUKO
Jamaa mmoja kutoka kaunti ya Bungoma huko Kenya amewashangaza wengi baada ya kudai kumsikia kuku akiwika tumboni mwake muda mfupi baada ya kusemekana kuwaiba kuku wanane.
Siku tatu baada ya kuwaiba kuku wanane, Mike Wanjala alisemekana kuanza kusikia maumivu na sauti ya jogoo kutoka tumboni mwake.
Wanjala alipata nafuu baada ya mamake kulipa pesa nyingi ili aweze kutibiwa na mganga baada ya jogoo kuwika kutoka tumboni mwake. Picha: TUKO
‘Nilianza kuhisi maumivu tumboni kabla ya kusikia jogoo akiwika kutoka tumboni mwangu kisha nikapelekwa kwa mganga kwa matibabu.’ Wanjala alielezea.
Haya yanajiri baada ya jirani yake kutafuta usaidizi kutoka kwa mganga anayejulikana kama ‘Mama Noor’
Baada ya kutibiwa, Wanjala alionywa na wakazi wa eneo hilo dhidi ya tabia yake ya wizi huku mamake akimshukuru mganga huyo kwa kumtibu mwanawe.
No comments :
Post a Comment