dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, September 22, 2016

JESHI LA POLISI LAONDOA ZUIO LA MIKUTANO YA NDANI YA VYAMA VYA SIASA!


Jeshi la polisi nchini limeondoa marufuku ya mikutano ya ndani kwa vyama vya siasa kwa madai kwamba limeridhishwa na hali ya kiusalama iliyopo nchini.

Hata hivyo, Kamishna wa operesheni na mafunzo, Nsato Marijani amesisitiza kwamba maandamano na mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa bado imezuiliwa isipokuwa kwa wabunge katika majimbo yao.

Ametoa wito kwa vyama vya siasa na wananchi wote kuheshimu sheria za nchi na kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo ili kuimarisha usalama wa raia na mali zao

"Maandamano na mikutano ya hadhara imezuiliwa hadi tathmini pana zaidi ya hali ya usalama itakapofanyika," amesema Marijani.

/Mwananchi

No comments :

Post a Comment