dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, September 16, 2016

MATUKIO YA BUNGENI MJINI DODOMA LEO!

 Spika wa Bunge la Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiingia katika ukumbi wa Bunge kuongoza kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge la Jmahuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha saba cha bunge la kumi na moja ambapo pia alisema kiasi cha shilingi milioni themanini na tano na laki tano zimechangwa kutokana na makato ya posho ya siku moja yawabunge kwa ajili ya kusaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
 Waziri wa Habari, utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (MB) akimueleza jambo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, kazi, Ajira, Vijana na watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (MB) picha juu ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akiteta jambo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki wakati wa kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo (MB) akijibu swali bungeni ambapo alisema kuwa serikali itaendelea kupeleka fedha katika serikali za mitaa kwa kuzingatia hali ya makusanyo ya kila mwezi.
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akijibu swali bungeni ambapo alitoa wito kwa wabunge kuisaidia kutoa elimu kwa wananchi waliovamia maeneo ya jeshi kuondoka ili kusaidia kupunguza migogoro ya ardhi baina ya jeshi na wananchi, wakati wa kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge akijibu swali bungeni ambapo alisisitiza kuwa Serikali inatekeleza program ya maendeleo ya Sekta ya maji kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo, wakati wa kikao cha saba cha Bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Jumanne Maghembe (MB) akimueleza jambo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula (MB), wakati wa kikao cha saba cha Bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
Mbunge wa Jimbo la Mikumi Mhe. Joseph Haule akiuliza swali bungeni kutaka kujua mikakati ya serikali katika kutatua migogoro baina ya wakulima na wafugaji inayopelekea mauaji ya raia ambapo Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi alisema Serikali itawachukulia hatua kali za kisheria wale wote wanaohusika na mauaji ya raia nchini hasa ikiwemo wanaohusika kwenye migogoro hii.
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO.

No comments :

Post a Comment