dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, September 14, 2016

MTANZANIA AKAMATWA MAREKANI KWA UTAPELI!

Image result for WILBROD FRANK LUKAMILWA

Wilbrod Frank Lukamilwa

Mtanzania Wilbrod Frank Lukamilwa alitiwa mbaroni siku ya Jumanne iliyopita Septemba 6, 2016 baada ya polisi wa kaunti ya Montgomery jimbo la Maryland kumtafuta zaidi ya mwaka bila mafanikio huku polisi ikiwa imetoa $10,000 kwa yeyote atayetoa taarifa zitakazowezesha kukamatwa kwake.

Wilbrod Frank Lukamilwa miaka 41, mkazi wa Takoma, Jimbo la Maryland siku hiyo ya Jumanne Polisi wa kauti ya Montgomery wakiwa mjini Silver Spring wakigawa vipeperushi vyenye picha yake kwa wapita njia, ndipo mtu waliyekua wakimtafuta zaidi ya mwaka alipopita mbele yao na yeye bado kidogo polisi hao wangemgawiya kipeperushi hicho.

Mmoja wa Polisi hao aliweza kumtambua kwa kumfananisha kwenye picha iliyokua kwenye kipeperushi na kumwita jina na yeye alipogeuka na Polisi kumkamata kirahisi.

Wilbrod Fank Lukamilwa ameshtajiwa na mtu mmoja ambaye anadai alimlipa pesa kwa ajili ya mafunzo ya awali ya chuo cha unesi baada ya Lukamilwa kujitambulisha kwake kuwa yeye ni mkuu wa chuo cha unesi cha hospitali na angeweza kumsaidia mtu huyo kujiunga na masomo ya unesi katika hospitali hiyo.

Mtu huyo inadaiwa kukutana na Lukamilwa mwaka 2012 na tangia mwaka 2015 polisi wamekua wakimtafuta Wlbrod Frank Lukamilwa bila mafanikio.

No comments :

Post a Comment