Hakuna taarifa zozote za matatizo kuhusu mahujaji wa Tanzania katika maeneo waliyofikia, wote wako salama na afya njema.
Mwaka huu Serikali ya Saudi Arabia imeimarisha miundo mbinu, usafiri, ulinzi, usalama na uangalizi makini kuhakikisha kuwa hakuna dosari zozote zinazoweza kutokea kutokana na uwepo wa wingi wa mahujaji kutoka nchi mbalimbali duniani.
Takriban mahujaji milioni 2 kutoka mabara yote duniani wapo nchini Saudi Arabia kutekeleza nguzo mojawapo kati ya nguzo 5 za dini ya kiislamu.
Taarifa imetolewa na:
Balozi Hemedi Iddi Mgaza
Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia
No comments :
Post a Comment