Watanzania wanaoishi Toronto, Canada, wamejumuika pamoja na kuunda timu yao ya kandanda inayojulikana kwa jina la Taifa Stars Toronto (TST).
Mazoezi yanaendelea chini ya kocha Falcao.
Watanzania hao wanasema kuwa wanategemea kukusanya vipaji vya aina yote kutoka kwa wazee na kwa vijana na kuweza kufanya mashindano na ndugu zao waliopo USA na kufanya Bonanza la hali ya juu kabisa kila mwaka katika wakati wa Summer.
Kama wewe unaishi Toronto au kwenye vitongoji vyake na unaliweza kandanda, basi wasiliana na blog lako la Zanzibar Ni Kwetu ili likuunge moja kwa moja na wahusika upate kuonyesha maajabu yako uwanjani.
Hivi juzi tu timu hii ilishiriki vizuri sana katika Youth East African Cup (Canada), lakini ushindi ulikuenda kwa timu ya Eritrea waliokinyakua kikombe.
No comments :
Post a Comment