dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, October 22, 2016

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AWATAKA WANAWAKE KUWAFICHUA WAPENDA RUSHWA WANAOKWAMISHA HARAKATI ZAO ZA KUJIKOMBOA KIUCHUMI!

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kongamano la pili la Sauti ya Wanawake Wajasiriamali Tanzania (VoWET) katika ukumbi wa PH Planes Quality Plaza, Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kongamano la pili la Sauti ya Wanawake Wajasiriamali Tanzania (VoWET) katika ukumbi wa PH Planes Quality Plaza, Dar es Salaam ambapo 

Makamu wa Rais aliwataka Wanawake wajasiriamali kuwafichua watendaji wa mamlaka za kurasimisha biashara watakaowadai rushwa wakati wa kupatiwa huduma ya kurasimisha biashira zao.

Makamu wa Rais alitoa wito huo leo jijini Dar es Salaam wakati kufungua Kongamano la Pili la Sauti ya Wanawake Wajasirimali Tanzania (VoWET).

Alisema wanawake hawapaswi kuogopa kuwafichua watendaji wanaowaomba rushwa kwani wanawakwamisha katika harakati zao (wanawake) za kujiendeleza kibiashara,kiuchumi na pia kukwamisha juhudi za serikali katika kuinua maendeleo ya Wanawake nchini.
Rais wa VoWET Bi. Maida Waziri (kulia) akihutubia wakati wa Kongamano la Pili la Sauti ya Wanawake Wajasiriamali Tanzania ambapo licha ya kupongeza jitihada za serikali ya awamu ya tano katika masuala mbali mbali ya kumuwezesha mwanamke pia alielezea changamoto ambazo wanawake wanakutana nazo katika shughuli zao za kuwainua kiuchumi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia baadhi ya kazi za ubunifu zilizofanywa na Wanawake Wajasiriamali kabla ya ufunguzi wa Kongamano la pili la Sauti ya Wanawake Wajasiriamali Tanzania (VoWET) katika ukumbi wa PH Planes Quality Plaza, Dar es Salaam.


No comments :

Post a Comment