dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, November 20, 2016

Jumla ya vijana 50 wameondoka nchini leo kuelekea nchini China kusomea kozi zifuatazo!

Jumla ya vijana 50 wameondoka nchini leo kuelekea nchini China kusomea kozi mbalimbali ikiwemo za afya na uhandisi katika masuala ya Petroli kwa ngazi ya shahada ya kwanza zikazochukua miaka minne na sita kutegemea na aina ya kozi.

Katika mahojino maalum yaliyofanyika uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere,Dar Es Salaam,muda mchache kabla ya kuanza safari yao itakayoawachukua maili nyingi kufika nchini China,wameelezea matumaini yao kuwa stadi na maarifa watakayokwenda kupata nchini humo katika shahada za udaktari na Upasuaji,Uhandisi wa masuala ya Petroli na usanifu majengo,vitakuwa na tija kwao na taifa kwa ujumla.

Miongoni mwa wasichana 20 kati ya vijana hao 50 wanaokwenda nchini humo,Monica Malugu na Anastacia Meresho,nao wamezunguzia matarajio yao ikiwemo mitazamo kuwa wanawake hawawezi masomo fulani kwakuwa ni magumu na katika haua nyingine,Glory Minja,mwakilisi wa Taasisi ya Universal Abroad Link (UAL),yenye dhamana ya kuwatafutia vyuo na ushauri kulingana na soko la ajira na kujiajiri,amesema,kila kiyu kiko sawa na kwamba wanasubiriwa kuanza masomo.

No comments :

Post a Comment