dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, November 7, 2016

Rais Dk Shein: Hakuna mahakama ya kunin’goa!

Image result for dr ali shein

  • Awataka wananchi kuendelea na shughuli zao bila ya hofu
  • Asema anaejua hatma yake sio mtu ni Muumba
Na Haji Nassor, Pemba
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi dk: Ali Mohamed Shein, amerejea kauli yake ya kuwataka wananchi kuendelea na shughuli zao za kujiletea maendeleo bila ya hofu, maana uchaguzi umeshamalizika na yeye ndie rais halali wa  Zanzibar, na wala hakuna mahakama yoyote duniani inayoweza kumng’oa.

Alisema wanaokwenda mashariki na magharibi ya dunia waendelee kufanya hivyo, na hata kuendelea kwenda kwenye mahakama ya kihalifu ya ICC, lakini amewahakikishia wananchi kuwa, hakuna uchaguzi mwengine hadi mwaka 2020.Dk: Shein ameeleza hayo kwa nyakati tofauti, mkoa wa kaskazini Pemba, alipokuwa akizungumza na wananchi wa wilaya ya Micheweni mara baada ya kutembelea ujenzi wa ukumbi wa halmshauri na ufunguzi wa skuli ya Maandalizi Junguni Gando.

Alisema yeye yupo madarakani kwa mujibu wa sheria na katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, na ameingia Ikulu baada ya wananchi kumpigia kura na kushinda kwa kishindo, hivyo kama kuna yoyote hakuridhishwa na hilo, aende mahakamani.

Dk: Shein amewataka wananchi hao wa Micheweni na Gando kuwapuuza wanaosema kuwa uchaguzi utarejewa au kuwa yeye hamaliza muda wake wa miaka mitano ijayo, kwa kisingizo cha kuwepo kwa mahakama ya kimataifa kumuondoa.

Rais huyo wa Zanzibar, amekuwa akirejea kauli hiyo mara kwa mara, ambapo aliwataka wananchi hao kuelewa kuwa, yeye ndie rais halali, na ameshawachagua mawaziri, makatibu wakuu na watendaji wengine na sasa kilichopo mbele yake ni kutekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020.

Alisema wapoa wanaopita pita na kuwaeleza wananchi kuwa rais wa Zanzibar hatomaliza muda wake wa uongozi na wakisambaaza maeneno kuwa, ataondolewa na mahakama za kimataifa.

Aliwaeleza wananchi hao, kuwa waendelee kuwapuuza wale wanaoutafuta urais wa Zanzibar nje nchi na hasa baada ya kushindwa kwa hiari zao, kuingia kwenye uchaguzi wa marudio wa mwezi Machi mwaka huu.  

“Wananchi ondoeni hofu, mimi ndie rais wenu, milionichagua Machi 20, mwaka huu, na wala hakuna mahakama wala mtu wa kuniondoa, na mwenye mamlaka ya kujua hatma ya umri ni Allah pekee’’,alifafanua.

Akizungumzia ukumbi huo wa Halmshauri ya Wilaya ya Micheweni, Dk: Shein amesema anaamini utatanua wigo wa kiuchumi na mapato kwa halmshauri hiyo.

Alieleza kuwa, ukumbi huo ambao ni wa kisasa, utatumiwa na hata wananchi wa kawaida, kwa shughuli zao mbali mbali ikiwa ni pamoja mikutano na harusi.

‘Ukumbi huu, nimeshaukagua na ni wakisasa, sasa hapa halmshauri itaongeza pato lake, lakini na nyinyi wananchi mtaumia kwa shughuli zenu’’,alifafanua.

Wakati huo huo rais huyo wa Zanzibar na Mwneyekiti wa baraza la Mapinduzi dk: Ali Mohamed Shein wakati akiizindua skuli ya Maandalizi ya Junguni Jimbo la Gando, amewataka wananchi kuwa karibu na watoto wao hasa wa maandalizi.

Alisema sera ya elimu ya mwaka 2006, imekuwa ikiweka mkazo umuhimu wa elimu ya maandalizi, maana hapo huandaliwa mwanafunzi kwa ajili ya elimu ya juu.

Katika hatua nyengine rais huyo wa Zanzibar, alisema kabla ya mapinuzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, hakukuwa na mtoto wa kinyonge alikuwa na uwezo wa kusoma elimu ya maandalizi, jambo ambalo kwa leo halipo.

“Azma ya rais wa kwanza wa Zanzibar wa kutangaaza elimu bure, imetusaidia sana leo hii, na ndio maana hata baada ya kuwepo kwa michango na sasa imeshafutwa kwa lengo lilelile ili kila mtoto mwenye uwezo wa kusoma apate elimu’’,alifafanua.

Mapema Katibu mkuu wizara ya nchi afisi ya Makamu wa Pili wa rais Zanzibar Abdalla Joseph Meza, alisema hadi kukamilika kwa jengo hilo la skuli ya maandalizi shilingi zaidi ya milioni 82 zilitumika, ikiwa nguvu za wananchi ni shilingi 11 na TASAF III ilichangia shilingi milioni 61.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Riziki Pembe Juma, aliipongeza serikali kwa juhudu zake za makusudi  katika kuchapuza maendeleo ya kielim siku hadi siku.

Akisoma risala ya wanacnhi wa shehia Gando, mwalimu Mkuu wa skuli ya Gnado  Mmaka Hamad Nassor, alisema baada ya kuona watoto wao wanahangaika, walifikia uamuzi wa kuanza kujenga skuli hiyo yenye madarasa matatu, na kisha TASAF III kuwaunga mkono.

Ujenzi wa skuli hiyi ilioanza mwaka jana, litatakuwa na uwezo wa kusomewa na wanafunzi 100 kwa wakati mmoja, ambapo hadi sasa skuli hiyo ya maandalizi ina mwalimu mmoja, huku rais wa Zanzibar akiiagiza wizara ya elimu kupeleka waalimu skulini hapo.

No comments :

Post a Comment