dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, July 30, 2017

Kim Jong-un: Tunaweza kushambulia eneo lolote Marekani!

Korea Kaskazini imesema kuwa imefanikiwa kufanyia jaribio kombora lake la masafa marefu ICBM, wakitaja kuwa onyo kali kwa Marekani.

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un alisema kuwa jaribio hilo lilibaini kwamba marekani yote ipo katik radara ya Korea Kakazini na sasa inaweza kushambuliwa, vyombo vya habari vimeripoti.

Jaribio la kombora hilo linajiri wiki tatu baada ya jaribio la kombora la kwanza la masafa marefu la Korea Kaskazini.

Rais wa Marekani Donald Trump amelitaja jaribio hilo kuwa la kijinga na kitendo cha hatari kilichotekelezwa na utawala wa Korea Kaskazini.China pia imeshutumu jaribio hilo huku ikitaka pandfe husika zilizo na waiwasi kujizuia ili kutoendeleza wasiwasi zaidi.

Ikithibtisha kurushwa kwa kombora hilo, Korea Ksakzini ilisema kuwa kombora hilo la masafa marefu liliruika kwa dakika 47 na kufika urefu wa kilomita 3,724.

Imesema kuwa jaribio hilo lilifanikiwa kujaribu uwezo wa kombora hilo kuingia, Kiongozi huyo pia alisema kuwa jaribio hilo lilithibitisha kwamba Korea Kaskazini sasa ina uwezo wa kushambulia ardhi yoyote ya Marekani kulingana na chombo cha habari cha Yonhap.

Taarifa hiyo ilisema kuwa kombora hilo ni Hwasong 14 kombora sawa na lile lililojaribiwa Julai 3.
Kombora hilo la masafa marefu lilisafiri kwenda juu ikilinganishwa na kombora lililorushwa Julai 3 hatua inayothibitisha kuwa taifa hilo linaweza kushambulia ndani ya Marekani.

Hatahivyo tathmini ya kikamilifu ikiwa bado haijafanikishwa mbali na muda uliochukuliwa na kombora hilo kuruka.

Muda mfupi baada ya jaribio hilo Korea Kusini, Japan na Maafisa wa Marekani waliripoti data kuhusu eneo na umbali, pamoja na muda uliochukuliwa na kombora hilo.

Ijapokuwa tathmini kamili haijakamilishwa, vitu kadhaa vilibainika, Kwanza, data iliopo inaonyesha kuwa kombora hilo lina uwezo wa kuruka umbali wa kilomita 10,400.

Kombora hilo linaweza kurushwa na kufika mji wa New York, Pili Marekani iliripoti kwamba Korea Kaskazini ilirusha kombora hilo kutoka Mupyong -ni Korea Kaskazini.

Eneo hilo lilikuwa tofauti ikilinganishwa na taarifa za awali ambazo zilifanikisha jaribio yaliotabiri kurushwa kwa kombora la Kusong.
Kombora hilo lilirushwa usiku wa saa tano ambao sio muda wa kawaida wa Korea Kaskazini , Inawezekana kwamba Korea Kaskazini ilijaribu kurusha kombora hilo usiku na hivyobasi kurusha makobora kadhaa ambayo yanaweza kuwachanganya waangalizi.

Ripoti siku ya Ijuma ilisema kuwa kombora hilo lilianguka katika bahari ya Japan, Kujibu hatua hiyo, Marekani na Korea Kusini zilifanya zoezi la pamoja la kijeshi kwa kurusha makombora ardhini kulingana na afisa mmoja wa idara ya ulinzi Marekani.

No comments :

Post a Comment