dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, July 27, 2017

Twaweza: Nusu ya Watanzania wako salama!

UTAFITI uliofanywa na taasisi ya Twaweza umeonyesha kuwa usalama kwa nusu ya Watanzania umeimarika katika mwaka mmoja uliopita kwa asilimia 53 ambapo asilimia 37 walisema hali ya usalama imebaki vilevile na asilimia 10 wanasema hali imekuwa mbaya zaidi.

Utafiti huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze, katika mkutano na wadau uliofanyika katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Dar, alipofafanua kuwa matokeo hayo yametokana na utafiti wake uitwao ‘Hapa usalama tu: Usalama, polisi na haki nchini Tanzania’.
“Muhtasari huu unatokana na takwimu zilizokusanywa kutoka sauti za wananchi, utafiti wa kwanza barani Afrika kwenye uwakilishi wa kitaifa unaotumia simu za mkononi.

Ni matokeo na takwimu zilizokusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,805 katika maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara bila kuhusisha serikali ya Zanzibar yaliyofanyika Aprili mwaka huu,” alisema.



No comments :

Post a Comment