dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, August 9, 2017

HEALTH: Faida Zitokanazo Na Matumizi Ya Mapapai!

ASILI ya mpapai ni Amerika ya Kati, ambapo kuanzia matunda, majani na utomvu wa mmea huu hutumiwa kama dawa maeneo mbalimbali duniani. Vile vile, matunda na utomvu wake yamekuwa yakitumika kutengeneza pombe na mvinyo katika baadhi ya nchi, huku wengine wakitumia mpapai kama dawa kwa mifugo na binadamu.

Inaelezwa kuwapo na tafiti zilizowahi kufanyika na kuchapishwa katika jarida lijulikanalo kwa jina la ‘Archieve’ la nchini India mnamo Oktoba 27 mwaka 2010, ambapo jarida hilo lilieleza kwamba juisi ya majani ya mpapai iliweza kusaidia wagonjwa watano waliowahi kupata homa ya dengue.

Mbali na utafiti huo, pia kuna tafiti zilizowahi kufanywa na madaktari wa nchini Marekani na Japani na kubaini kuwa, juisi ya majani ya mpapai ina uwezo wa kutibu malaria na saratani, japokuwa tafiti hizo hazikukubawaliwa kisayansi.
Faida za kiafya za tunda la papai.Aidha, wataalam wa lishe nao wanaeleza kwamba, watu wenye matatizo ya kupatwa na majipu, uvimbe na vidonda mara kwa mara huwa na upungufu wa virutubisho muhimu, ambavyo huweza kupatikana ndani ya papai, hivyo imegundulika watu wenye matatizo hayo wakitumia papai hupata nafuu na kupona haraka.

Pia papai husaidia kuleta nuru ya macho, kama inavyoaminika kwa karoti, hali kadhalika papai pia husaidia kupunguza madhara yatokanayo na moshi wa sigara.

Hivyo wavutaji wa sigara ni vyema wakatumia tunda hili mara kwa mara ili kujipunguzia madhara ya moshi wa sigara, ingawaje ni vyema wakakumbuka matumizi ya sigara si mazuri kwa afya hivyo ikibidi ni vizuri kuacha kabisa.

Ni wazi kuwa papai ni tunda lililosheheni kila aina ya utajiri wa vitamin kuliko matunda mengine, kwani lina vitamin A, B, C, D na E.

Wataalam wa tiba za asilia pia wanaeleza kwamba tunda hili linauwezo wa kutibu tatizo la usagaji wa chakula tumboni pia hutibu kisukari na pumu na mara nyingine hata kifua kikuu.

Tunda la papai lina faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Miongoni mwa faida hizo ni pamoja na kuwa na uwezo wa:

  • Kutibu tatizo la Shida ya kusaga chakula tumboni
  • Kutibu Udhaifu wa tumbo
  • Kutibu Kisukari na asthma au pumu.
  • Kutibu Kikohozi kitokacho mapafuni
  • Kutibu Kifua kikuu
  • Tunda hili huleta afya nzuri ukitumia kila siku
  • Maziwa yanayotoka katika jani lake huponya vidonda
  • Vilevile yanasaidia kutibu sehemu palipoungua moto
  • Kama hiyo haitoshi, maziwa yanayotoka katika jani la mpapai yanatibu kiungulia na Ugonjwa wa colon (njia ya haja kubwa ndani)

Pia yanasaidia kutofunga choo
Maganda ya tunda la papai yanasaidia kutibu tatizo la kuungua, vipele na saratani ya ngozi.
Mbegu zake zinatibu ini zikitafunwa 10 – 12 kwa siku 5.
Majani yake yakaushie ndani, yanatibu pumu. Inapoanza kubana yachome majani yaliyokaushwa kisha jifukize, kule kubanwa kutakisha.
Majani yake yanasaidia katika kutibu shinikizo la damu.
Papai likimenywa na kupondwa linafaa Sana katika masuala ya urembo kwani linaweza kutumika Kama vile unavyotumia lotion kulainisha uso.
Mbegu za papai zina uwezo wa kutibu homa. Meza mbegu za papai kiasi cha kijiko cha chakula mara 3 kwa ajili ya kutibu homa.
Mbegu za papai zilizokaushwa ndani kisha zikasagwa kuwa unga zinatibu malaria, tumia kijiko 1 cha chai changanya na uji, kunywa mara 3 kwa siku 5 Mgonjwa wa kifua kikuu akila matunda haya kwa muda mrefu atapona bila dawa nyingine.
Mizizi yake ikipondwa na kulowekwa katika maji yaliyochemshwa, lita 2 na nusu kwa dakika 15, yanatibu figo, bladder, yanazuia kutapika. Nusu kikombe cha chai kutwa mara 3 kwa siku 5.

Tikiti maji
TIKITI MAJI ni moja ya matunda yanayolimwa sana katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania tofauti na miaka iliyopita.Hii inaashiria kwamba tunda la tikiti maji linaliwa sana katika maeneo hayo kutokana na faida inayopatikana kwenye tunda hilo.

Faida ya kutafuna mbegu za tikiti maji
Pamoja na kuongezeka kuliwa kwa tunda la tikiti maji lakini wengi wa wateja wanaokula tunda hilo huwa hawajui faida ya mbegu za tunda hilo.Kutokana hali hiyo wengi wanaokula tikiti maji wanatema mbegu hizo na huenda wengi walikuwa na imani potofu inayokataza kula mbegu za tunda.Hivyo badala ya kuzitafuna mbegu hizo wengi huzitema na kuona ni kitu kisicho na faida yoyote katika mwili wa binadamu.

Lakini mbegu hizo zinatakiwa kutafunwa wakati unapokula tunda lenyewe na hii ni kutokana na faida zake kiafya.Unapokula tunda la tikiti maji unachotakiwa kufanya ni kuzitoa mbegu zake na kuziweka kwenye chombo kimoja mpaka zichipue yaani kuanza kutoa mizizi.

Baada ya hapo unatakiwa uzikaushe tayari kwa kuzitumia kutoka na faida hizi zifuatazo: Mbegu za tikiti maji zina protini nyingi hivyo kuzitafuna kunaweza kumpatia mlaji chanzo cha protini.Pia aunzi mmoja tu (takriban ujazo wa 1/8 wa kikombe) inakupa virubutisho vya protini vya gramu 10.

Hii ni sawa sawa na kiwango kinachopatikana kutoka katika yogati ya Kigiriki wakati wa kustaftahi. Mbegu ‘zilizochipua’ zimemea na mara nyingi zina virutubisho vya hali ya juu kuliko zile ambazo hazichipua.Kuchipua kunaondoa mchanganyiko katika chakula ambacho husababisha ugumu wa kufyonza virutubisho vyote.

Mbegu za tikiti maji zilizochipua zikitafunwa huongeza msongamano wa virutubisho na kusababisha urahisi kumeng’enya chakula. Kuhusu tikitimaji, mbegu hutolewa ngozi nyeusi ya juu na kubaki ikifanana na mbegu zilivyo.Katika mbegu za zamani hili halipatikana lakini umegundulika kwamba kweli mbegu hizi zinaleta afya kwenye mlo.

Mbegu za tikiti maji zilizochepua zina protini, vitamin B, Magnesia, na mafuta ambayo hayakoleza.Wataalamu wa masuala ya chakula wanasema mafuta yaliyokolezwa mara nyingi hayana viwango vya lehemu na muasho na yanaondoa hatari ya kupata ugonjwa wa moyo na kiharusi.

Kama umeshawahi kutafuna mbegu za matikiti maji wakati ukila tunda hilo uligundua ladha yake ni sawa na tunda lenyewe. 
Mbegu za matikiti maji ni sawa na mbegu za alizeti kwa ladha, lakini haina lozi kubwa. 

Zinakuwa na ladha nzuri zaidi zikiwa kwenye kachumbari, iliyochanganywa pamoja au ukiila ikiwa mkononi mwako.

Jungu na mbegu nyingi ni nzuri kwa mwili wa mwanadamu, lakini ukilinganisha ukubwa wa lishe unaopatikana basi mbegu za matikiti maji
Kama vile haitoshi tunda hili limejaaliwa virutubisho kadha wa kadha vyenye faida kubwa katika afya ya mwanadamu.

Licha ya 92% ya tikiti maji kuwa ni maji, bado zile 8% zilizobaki zina faida kubwa sana kiafya jambo linaloonekana kutofahamika kwa wengi. Zifuatazo ni baadhi tu ya faida chache kati ya nyingi za tunda hili la tikiti maji:

Tikiti maji ni chanzo kizuri cha vitamini. Katika tunda hilo kuna Vitamin A, inayosaidia kuboresha afya ya macho na pia kuondosha sumu mwilini; Vitamin C, inayosaidia kuboresha kinga, kuponya majeraha, kukinga uharifu wa seli, kuboresha afya meno na fizi; na vitamini B6, inayosaidia ubongo kufanya kazi na pia kuibadilisha protini kuwa nishati.

No comments :

Post a Comment