dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, August 11, 2017

UCHAGUZI KENYA: Wafuasi wa wagombea wakabiliana Garissa!

Sehemu ya soko kuu mjini Garissa, kaskazini mashariki mwa Kenya, imeteketea baada ya mfarakano kati ya wafuasi wa wagombea wawili wa ugavana katika kaunti hiyo.

Fujo zilizuka baada ya matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika Jumanne kutangazwa.

Ali Bunow Korane wa chama cha Jubilee chake Rais Kenyatta alitangazwa mshindi.

Taarifa zinasema watu wasioridhishwa na matokeo hayo walichoma moto sehemu za soko hilo.

Hali ya utulivu imerejea lakini wazima moto wameendelea kukabiliana na moto huo.

Korane alipata kura 55 335 (51,48%) naye mpinzani wake wa karibu Nathif Jama Adan wa chama cha Wiper akapata kura 50 471 (46,95%).

Bw Adan ndiye gavana anayeondoka.




No comments :

Post a Comment