dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Thursday, June 7, 2018

MAMBA AUA MCHUNGAJI AKIBATIZA WAUMINI ZIWANI!

Habari kutoka Kusini mwa Ethiopia zinasema kwamba mchungaji ambaye alikuwa akiendesha ibada ya kubatiza waumini ufukweni mwa ziwa amefariki baada ya kushambuliwa na mamba wakati akibatiza.
Mchungaji huyo ambaye ametambuliwa kwa jina la Docho Eshete alikuwa akiendesha ibada hiyo ya waumini 80 siku ya Jumapili iliyopita katika ufukwe wa Ziwa Abaya katika mji wa Arba Minch wilaya ya Merkeb Tabya.

Wakazi wa mji huo waliliambia shirika la utangazaji la BBC kwamba Mamba huyo aliruka kutoka ndani ya maji wakati mchungaji huyo akiwabatiza waumini na kumng'ata miguu,mgongo na mikono majeraha yaliyosababisha kifo chake.

No comments :

Post a Comment