dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, July 6, 2018

Watanzania wataka vyama vya upinzani viruhusiwe kufanya mikutano!

Utafiti wa taasisi ya 'Twaweza Ni Sisi' uliotolewa leo umeonyesha kuwa Watanzania asilimia 64 ya  wanataka vyama vya upinzani viruhusiwe kufanya mkutano ya hadhara jambo ambalo ni tofauti ukilinganisha na asilimia 51 ya mwaka 2016.

Ripoti hiyo iliyotolewa leo jijini Dar es salaam imeonyesha watu watano kati ya 10 wanapinga katazo la mikutano hiyo sawa na asilimia 48 huku watu wanne kati ya 10 wakiunga mkono.Ripoti hiyo imesema kwamba suala la uwajibishwaji utafiti huo uliofanywa na Twaweza ni Sisi unaonyesha asilimia 59 ya Wananchi wanataka Rais awajibishwe na Bunge kutoa maelezo ya matumizi ya fedha za walipa kodi.

“Asilimia 78 ya wananchi wanataka Rais aheshimu sheria na matumizi ya mahakama," umesema utafiti.

Aidha katika utafiti huo umeonyesha kushuka kwa uungwaji mkono wa CCM vijijini ikiwa na maana kwamba uungwaji vijijini ni 59% na mijini 56%.

No comments :

Post a Comment