dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, July 6, 2018

Zitto, Lema, Mtatiro, Polepole, Nape watoa neno kutumbuliwa kwa Mwigulu!


BADA ya Rais Magufuli kutangaza mabadiliko madogo katika Wizara kadhaa na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba kuachwa, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole na Kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe wameanza kuvutana mitandaoni kuhusu kuachwa kwa Mwigulu.Kupitia mtandao wa wa Twitter Zitto Kabwe amemkaribisha, Dkt. Nchemba kwa kumwambia sasa ni wakati wake wa kuwatumikia wananchi na kwamba msimamo wake ndiyo uliomponza.
Kufuatia kauli hiyo, Humphrey Polepole katika ukurasa wake, ameamua kumvaa Kiongozi huyo wa ACT kwa kumuita mzee wa kurukia treni kwa mbele  na kwamba Rais amefanya mabadiliko kutokana na dhamana aliyopewa na Katiba na si vinginevyo na kumtaka asipotoshe watu.
Kwa upande wa Mbunge wa Mtama ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Habari, Sanaa, Michezo na Utamaduni, Nape Nnauye amemkaribisha kiongozi huyo na kumtaka waungane kuwatumikia wananchi.

Lema na Mtatiro wafunguka:

No comments :

Post a Comment