dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, August 12, 2018

Jumuiya ya Afrika Mashariki kuanza kufanya doria ya pamoja!


Nchi tatu za Jumuiya za Afrika Mashariki, Tanzania, Kenya na Uganda zimeanza makubaliano ya kufanya doria maeneo ya mipakani ili kudhibiti mianya ya biashara za magendo ambazo zinahatarisha soko la bidhaa za ndani pamoja na uingizwaji wa bidhaa zisizo na ubora kutoka nje ya nchi.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw.Charles Kichere ameyasema hayo wakati akikagua njia za panya katika  mipaka ya Kamwanga, Tarakea na Holili zilizopo katika wilaya ya Rombo inayopakana na nchi jirani ya Kenya.Amesema kwa sasa mamlaka ya mapato Tanzania kwa kushiriana na mamlaka ya mapato ya Kenya watafanya mawasiliano na makubaliano ya kufanya msako mkali wa doria saa ishirini na nne maeneo ya mipakani kwa lengo la kudhibiti wafanyabiashara za magendo ambao wanakwepa kulipa kodi.

Nao Maafisa wafawidhi wa forodha za Tarakea na Holili wamesema changamoto kubwa zinazowakabili katika utendaji wa kazi maeneo ya mipakani ni pamoja na uhaba wa magari ya kufanyia doria mipakani, mashine za kukagulia mizigo.

No comments :

Post a Comment