Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Watu wa Zanzibar Limited Mhe. Kidawa Hamid Saleh, akizungumza na waandishi wa habari na kusisitiza jambo kuhusiana na changamoto zinazotokea katika utendaji wa huduma za kibenki kwa wateja wao.
Akizungumza na wajumbe wa bodi hiyo, katika hafla iliyofanyika ukumbi wa Benki ya watu wa Zanzibar, Mperani Mwenyekiti wa bodi hiyo, Kidawa Hamid Saleh alisema uimarishaji huo utasaidia kupunguza changamoto zinazoikabili benki hiyo.
Hata hivyo, alisema ni vyema kwa wafanyakazi kuongeza bidii katika uwajibikaji na kuendelea kuwa waadilifu ili wafanikishe malengo yabenki hiyo ambayo aliitaja kuwa tegemeo kwa wananchi.
Aidha, aliwataka wajumbe hao kutoa huduma bora kwa wateja wao kwa vile Zanzibar ina benki nyingi zinazotoa huduma kwa wanachi.
Sambamba na kuongeza kuwa katika kuhakikisha huduma zinapatikana, watatumia mawakala katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kufikisha huduma karibu kwa wananchi.
Hata hivyo, Mwenyekiti huyo alihimiza ushirikiano kwani alieleza kuwa ndio msingi ambao utailetea mafanikio benki hiyo pamoja na kuhakikisha wateja wanapata huduma bora.
Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Juma Ameir Hafidh alisema wanampango wa kuanzisha matawi mapya na kutoa huduma kupitia wakala ili kurahisisha huduma kwa wananchi.
No comments :
Post a Comment