dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, June 16, 2013

Uongozi ni dhamana ya kuwatumikia Wananchi – Balozi

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akifungua Semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi  inayofanyika huko Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akifungua Semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi iliyofanyika huko Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Viongozi wa Serikali na wale wa Kisiasa wanapaswa kuzielewa vyema sheria za Utawala ili waweze kutumia vizuri  madaraka yao na kwa uadilifu katika kuwahudumia wananchi wanaowasiamia na wale wanaowaongoza.
 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati akiifungua Semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi inayofanyika katika ukumbi wa Zanzibar Beach Resort uliopo Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
 
Balozi Seif alisema ufahamu mzuri wa Sheria za Utawala utawezesha  kuelewa kuwa madaraka yoyote waliyonayo Viongozi  hao wanayatumia kwa maslahi ya umma na kwa mujibu wa Sheria.
Alisema utekelezaji wa shughuli za kila muhimili unaweza kudhoofisha uhusiano mzuri baina ya mihimili  iliyopo Nchini endapo utakosekana ufahamu wa sheria na kupelekea migongano na mivutano kati ya Baraza la Wawakilishi na Taasisi za Serikali.
 
Balozi Seif alitahadharisha kwamba hatua hiyo kwa kiasi kikubwa inaweza kupotosha lengo la mgawanyo wa madaraka ambalo ni kuwapatia mafanikio na maendeleo Wananchi walio wengi hapa Nchini.“ Haitakuwa jambo la busara endapo Kiongozi yeyote yule atachukua msimamo wa kutekeleza majukumu yake kwa namna itakayohatarisha amani ya Nchi au kuvuruga Umoja tulionao “. Alisisitiza Balozi Seif.
 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwanasihi washiriki wa semina hiyo   kuzingatia daima kuwa Uongozi ni dhamana ambayo inapaswa kutumika kwa faida ya Nchi na Wananchi.
“ Viongozi tusitumie vibaya dhamana tulizopewa kwa kuvuruga mahusiano mazuri yaliyopo baina yetu au kwa kutumia vibaya vyeo vyetu dhidi ya watu wasiostahiki kufanyiwa dhulma hizo “. Aliongeza Balozi Seif.
 
Alilishukuru Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa  { UNDP } pamoja na Uongozi wa Baraza la Wawakilishi kwa kuridhia semina hiyo ifadhiliwe kupitia program ya kufadhili Mabunge licha ya kuwa semina hiyo haikuwemo katika shughuli zilizopangwa kwa robo ya Mwaka.
 
Alisema Serikali imejiwekea utaratibu wa kufanya semina mbali mbali kwa Viongozi wa Kisiasa na Kiutendaji kwa shabaha ya kukumbushana kuhusu majukumu na wajibu wa msingi walionao Viongozi katika kuwatumikia Wananchi.
 
Naye Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mh. Pandu Ameir Kificho alisema kwamba mamlaka ya kuendesha Nchi yako kwenye dhamana ya  Wananchi wenyewe na Kiongozi au Mtu aliyepewa  jukumu la kusimamia ya Jamii aelewe kuwa amebeba dhima hiyo.
 
Mh. Kificho ambae ni Mwenyekiti Mwenza wa Semina hiyo aliishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa wazo lake la kuandaa semina iliyowakutanisha Viongozi wa Serikali na Siasa ambayo ni muhimu  kwa hatma njema ya Wananachi wa Zanzibar.
 
Akitoa salamu za Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mtaifa { UNDP } lililodhamini Semina hiyo Naibu Mkurugenzi wa Shirika hilo Nchini Tanzania Bibi Andisa Mashologu alisema Shirika hilo litaendelea  kuunga mkono harakati za Kijamii  katika kuwajengea uwezo Wananachi katika mipango yao ya Maendeleo.
 
Bibi Andisa alisema  hatua hiyo itasaidia kujenga utulivu miongoni mwa Wananchi na viongozi wao na hatimae kutanuka zaidi kwa Demokrasia  kati ya makundi ya watu wa rika na itikadi tofauti Nchini.
 
Semina hiyo ya siku mbili  ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi imebeba mada nane ikiwemo jukumu la Baraza la Wawakilishi katika kusimamia Serikali.
 
Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Mapango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa  Nchini Tanzania Bibi Andisa Mashologu akitoa salamu kwenye semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi  inayofanyika huko Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Mapango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa Nchini Tanzania Bibi Andisa Mashologu akitoa salamu kwenye semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi inayofanyika huko Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Mahadhi Juma Maalim akitoa mada  inayohusu Jukumu la Baraza la Wawakilishi katika kusimamia Serikali kwenye semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi  inayofanyika huko Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Mahadhi Juma Maalim akitoa mada inayohusu Jukumu la Baraza la Wawakilishi katika kusimamia Serikali kwenye semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi inayofanyika huko Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Jaji Mkuu wa Zanzibar Mh. Omar Othman Makungu akitoa mada inayohusu  Katiba na Mgawanyo wa Madaraka katika mihimili ya Dola kwenye semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi  inayofanyika huko Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Jaji Mkuu wa Zanzibar Mh. Omar Othman Makungu akitoa mada inayohusu Katiba na Mgawanyo wa Madaraka katika mihimili ya Dola kwenye semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi inayofanyika huko Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Mawaziri wa SMZ walioshiriki Semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi  inayofanyika huko Zanzibar Beach Resort Mbweni. Kutoka kulia kuelekea kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali  Mh Ali Juma Shamuhuna  na Waziri wa Ardhi, Makazi, Maji na Nishati Mh. Ramadhan Abdulla Shaaban.
Mawaziri wa SMZ walioshiriki Semina ya siku mbili ya kuimarisha uhusiano baina ya Viongozi wa Kisiasa na watendaji kutoka Serikalini na Baraza la Wawakilishi inayofanyika huko Zanzibar Beach Resort Mbweni. Kutoka kulia kuelekea kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Mh Ali Juma Shamuhuna na Waziri wa Ardhi, Makazi, Maji na Nishati Mh. Ramadhan Abdulla Shaaban.
 Chanzo: ZanzibariYetu

No comments :

Post a Comment