dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Monday, July 31, 2017

Darasa la saba 400 kuondolewa kazini Morogoro!

Zaidi ya Wafanyakazi 400 wa Serikali wanatarajia kuondolewa kazini mkoani Morogoro kutokana na kushindwa kujiendeleza kielimu baada ya kuajiriwa miaka 13 iliyopita wakiwa na vyeti vya elimu ya msingi.
Watumishi hao ambao wengi wao ni wauguzi, wahudumu wa afya, madereva, wahudumu wa ofisi, watendaji wa mitaa, vijiji na kata tayari wamenyimwa mishahara yao ya mwezi huu.
Akizungumzia zoezi hilo aliyekuwa Mtendaji wa Kata ya Kimamba wilayani Kilosa, Mashaka Motile amesema katika wilaya hiyo watumishi zaidi ya 80 wamenyimwa mshahara bila maelezo yoyote na walipofuatilia ndipo walipofahamishwa kuwa walipewa muda wa kujiendeleza na wameshindwa kufanya hivyo.
“Hakuna barua yoyote tuliyopewa ya kusimamishwa kazi ila mshahara wa Julai hatujapewa na tulipofuatilia tuliambiwa kuna waraka wa Serikali unaosema wale wote walioajiriwa kuanzia mwezi Mei 20, 2004 wakiwa na elimu ya msingi na wameshindwa kujiendeleza wanatakiwa kuondolewa,” amesema.
Motile anasema yeye na baadhi ya watendaji wengine walisimamishwa kazi kimakosa kwani agizo linasema wasimamishwe kazi walioajiriwa kuanzia Mei 20, 2004 lakini wao waliajiriwa Mei Mosi, 2004.
Akizungumzia uamuzi huo wa Serikali, mhudumu wa afya wa manispaa ya Morogoro ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema uamuzi huo umekuwa wa ghafla mno na haujatoa muda wa wao kujiendeleza.
“Naiomba serikali ituongeze japo miaka mitatu ili tuweze kujiendeleza maana hivi tulivyosimamishwa kazi ghafla familia zetu zitaathirika sana na kuna hatari ya watoto wetu kuacha shule, tunaomba tuongezewe muda,” amesema.
Alipotakiwa kuzungumzia zoezi hilo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Kilosa, Kessy Mkambala alisema bado zoezi linaendelea litakapokamilika ndo ataweza kulizungumzia.
Naye Katibu wa Chama Cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) mkoani Morogoro, Lawrence Mdega amesema wamepokea malalamiko toka kwa wafanyakazi zaidi ya 150 wanaolalamika kuondolewa kwa kuwa wana elimu ya msingi.
“Nimeshawasilisha haya malalamiko makao makuu ya TALGWU ili washughulikie lakini tunachotaka watumishi hawa walipwe mshahara wa Julai ambao tayari waliufanyia kazi lakini pia walipwe mafao yao maana waliitumikia Serikali kwa uadilifu na vyeti vyao hivyo vya elimu ya msingi.

No comments :

Post a Comment