dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, July 8, 2017

MASAUNI AWAASA MADEREVA KUZINGATIA SHERIA ILI KUEPUSHA AJALI ZA BARABARANI!

 Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akiongoza maandamano ya Mabalozi wa Usalama Barabarani kuingia Uwanja wa Mashujaa, wakiadhimisha siku yao iliyofanyika kitaifa mkoani Dodoma leo.Kulia ni Katibu Mtendaji wa baraza hilo,Mkuu wa  Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,DCP Mohamed Mpinga. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni,akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani ambapo aliwaasa madereva kufuata sheria ili kuweza kupunguza tatizo la ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na kuacha idadi kubwa ya wahanga wa ajali  hizo.Wapili kushoto ni Katibu Mtendaji wa baraza hilo,Mkuu wa  Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,DCP Mohamed Mpinga na anayefuatia ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma,Lazaro Mambosasa. Maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa Uwanja wa Mashujaa, leo mkoani Dodoma.
 Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambae pia ni Mkuu wa  Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,DCP Mohamed Mpinga, akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani ambapo aliwaasa askari wa usalama  barabarani kusimamia sheria ili kuweza kupunguza tatizo la ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na kuacha idadi kubwa ya wahanga wa ajali  hizo.Kulia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na kulia ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma,Lazaro Mambosasa. Maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa Uwanja wa Mashujaa,leo mkoani Dodoma.
 Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani ambapo aliwashukuru mabalozi hao kuchagua mkoa wa Dodoma kufanyia maadhimisho hayo na kuahidi kuelimisha watumiaji wa vyombo vya moto sheria na kanuni za usalama barabarani ikiwa anaongoza mkoa ambao ni Makao Makuu ya nchi .Wakwanza kushoto  ni Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambae pia ni Mkuu wa  Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,DCP Mohamed Mpinga.Maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa Uwanja wa Mashujaa,leo mkoani Dodoma. 
 Mabalozi wa Usalama wa Barabarani wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani ambapo aliwaasa madereva kufuata sheria ili kuweza kupunguza tatizo la ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na kuacha idadi kubwa ya wahanga wa ajali hizo. Maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa Uwanja wa Mashujaa,leo mkoani Dodoma.
 Msanii Faustine Matina ambae ni Balozi wa Usalama Barabarani, akiimba wimbo wa kuhimiza masuala ya kuzingatia sheria za usalama barabarani wakati wa Siku ya Maadhimisho ya Mabalozi wa Usalama Barabarani, iliyofanyika kitaifa leo katika Uwanja wa Mashujaa,mkoani Dodoma.
 Mhanga wa ajali anayefahamika kwa jina la Mpemba Asilia, akizungumza na Mabalozi wa Usalama Barabarani, alipofika katikaMaadhimisho ya Mabalozi wa Usalama Barabarani yaliyofanyika kitaifa leo katika Uwanja wa Mashujaa,mkoani Dodoma.
Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(watano kulia),akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mabalozi wa Usalama Barabarani wakati wa  Maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani yaliyofanyika kitaifa Uwanja wa Mashujaa,leo mkoani Dodoma.Wasita kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambae pia ni Mkuu wa  Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,DCP Mohamed Mpinga.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

No comments :

Post a Comment