AirFreight

Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, February 22, 2026

SHULE 10 ZENYE ADA GHALI ZAIDI TANZANIA!

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Future Media imetoa orodha ya shule zenye Ada ghali zaidi hii, Aidha wamesema gharama hizo hazizingatii ada peke yake bali pia michango mingine mbalimbali ambayo wazazi na walezi hupaswa kuchangia kwa viwango mbalimbali katika shule hizi. Hebu twende tukatazame Kwa kina.

10. Morogoro International School (MIS)
Hii inapatikana mkoani Morogoro na hufuata mtaala wa Cambridge. MIS hutoza kuanzia Shilingi za Kitanzania milioni 6.4 kwa chekechea hadi shilingi za Kitanzania milioni 18 kwa sekondari. Hii ni ada peke yake, mbali na fedha ya usajili na boarding kwa wale wanaolala shuleni.

9. International School Moshi (ISM)/ UWC East Africa
Hii ndio shule ghali zaidi katika mkoa wa Kilimanjaro. Hutoza ada kuanzia shilingi za Kitanzania milioni 16 kwa chekechea hadi shilingi za Kitanzania milioni 41 kwa wale wa kidato cha tano na sita. Shule hii hufuata Mtaala wa International Baccalaureate (IB).

8. Aga Khan Primary & Secondary School
Shule hii iko katika Jiji la Dar Es Salaam, na hufuata Mtaala wa IB kama ilivyo ISM. Hutoza ada kuanzia Shilingi za Kitanzania milioni 7 hadi milioni 20.

UNAUA FIGO ZAKO KWA TABIA HIZI 10, Prof. JANABI ANABAINISHA!