dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, January 26, 2013

MASASI NAYO YAWAKA MOTO!

MTWARA YOTE SASA YAWAKA MOTO!


Update:
Nyumba ya Mkuchika inawaka moto-Newala

Taarifa za redio mbao sasa  ni kwamba wananchi wanaendelea kufanya
uharibifu mkubwa huko ambapo naambiwa wamevamia gereza wakafungulia
wafungwa na kisha kupiga moto gereza. Polisi wamezidiwa na
wamejifungia kituoni wanarusha mabomu yao tokea huko walikojificha
maana nje hakutamaniki. Na wameshateketeza nyumba ya mama Anna
Abdallah.

Update:
Kikao cha dharura cha kamati ya ulinzi na usalama kinaendelea kwa
kuwashirikisha maafisa wa polisi na maafisa usalama waliotoka Dar es
Salaam kuongezea nguvu.

Maaskari na makachero wawasili  Mtwara leo asubuhi na helkopta
kuongezea nguvu.

Hosteli ya wanafunzi wa chuo cha Utumishi maeneo ya Kiyangu B Mtwara
yakoswa koswa kuchomwa moto kwa kile kinachodhaniwa kuwa na uhusiano
na Hawa Ghasia mpaka sasa wanafunzi hawana mahala pa kukaa.  Kituo
kidogo cha Polisi Cha Shangani mkoani Mtwara nacho chakoswa na moto.
Ofisi ya Afisa Mtendaji Nkanaledi mkoani Mtwara nayo yavunjwa.

Wananchi wamechoma moto mahakama ya Mwanzo na kuvunja vioo vya nyumba
za waheshimiwa Hawa Ghasia (Waziri, TAMISEMI) na ya Mohamed Sinani
(Mwenyekiti wa CCM Mkoa) zilizopo mtaa wa Sinani.

Wakiwa katika mahakama ya mwanzo, Polisi walizingirwa na vijana
waliokuwa wamebeba mawe na kufunga barabara zote za kuingia na kutoka
Kituo Kikuu cha Mabasi na eneo la Soko Kuu, licha ya kufyatua hewani
mabomu ya machozi.

Baadhi ya barabara za zimezibwa kwa kuchomwa matairi ya gari, na
kuongeza hofu kwa wananchi.

Hali imeshakuwa mbaya masasi taarifa zilizotufikia punde wamechoma
eneo linaloitwa loliondo, ofisi za elimu na ofisi ya trafiki,
inasemekana jamaa wameshavamia ofisi za halmashauri wengine wako
njiani nyumbani kwa mama Ana Abdala, hapa Mtwara  mjini maduka yote
eneo la soko kuu na stendi yamefungwa hakuna huduma, huko Newala , leo
kuna mkutano mkubwa mchana huu wa kumkataa George Mkuchika.

Vurugu zahamia wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Nyumba ya Mbunge wa
Masasi nayo yateketezwa kwa Moto hivi sasa...Madereva Bodaboda
waandamana ...Vurugu zashamiri Mabomu Kibao..Hali ni tete

POLISI jana  wamelazimika kupiga mabomu ya machozi kutwa nzima katika
kata ya Chikongola, Manispaa ya Mtwara Mikindani kutawanya wananchi
walioizingira nyumba ya diwani wa kata hiyo Mohamedi Chehako kwa madai
ya kuwahifadhi wachawi ndani ya nyumba yake, huku mwandishi wa habari
mmoja akiripotiwa kujeruhiwa.

Habari ambazo hazijathibitishwa na kamanda wa polisi mkoani hapa,
Maria Nzuki zinadai kuwa majira ya saa 10 kasoro za jioni watu
wanaodaiwa kuwa ni wanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)
waliingilia kati na kuanza kutembeza mkong’oto kwa wananchi ili kuzima
vuguvugu hilo.

Mwandishi wa habari hizi alipojaribu kuwasiliana na kamanda Nzuki kwa
njia ya simu za mkononi hakuweza kupatikana.

Wananchi walitoa tuhuma hizo baada ya kukuta ungo ikiwa na tunguri
ndani yake ambayo inadaiwa kuwa ni ndege ya wachawi uwanjani kwake
maeneo ya makaburi Msafa.

Wananchi walijikusanya nyumbani kwa Diwani huyo na kumshinikiza awatoe
wachawi nje ili waweze kuwadhibu, amri iliyopingwa na Diwani huyo.
Kadiri mda ulivyokwenda ndivyo wananchi walivyozidi kuongezeka na
hatimaye kulijitokeza kundi la watu walioanza kutia vurugu, hali
iliyomlazimu Chehako kuomba msaada wa polisi.

Mashuhuda wa tukio walimweleza mwandishi wa habari hizi kuwa polisi
walipofika waliwasihi wananchi kutawanyika kwa kuwa ungo na tunguri
zake zilikuwa zimeteketezwa kwa moto na diwani huyo mbele ya wananchi
hao.

Chehako akihojiwa nyumbani kwake alisema: “Wananchi waliendelea
kupinga na kudai ndani ya nyumba kuna rubani na abiria wa ndege
nimewahifadhi…polisi wakawachagua wananchi watano na kuingia ndani ya
nyumba kuwasaka watu hao…hawakuona kitu, walitoka nje na kuwamabia
wenzao hata hivyo wenzao walibisha.

Walianza kurusha mawe nyumba… polisi walianza kupambana nao kwa
kuwarushia mabomu…hata hivyo wananchi walikuwa wanakimbia na kwenda
upande wapili kufanya vurugu.”

Chehako alibainisha kuwa ni kawada yake kuamka alfajiri kwa ajili ya
sala ya asubuhi, lakini asubuhi ya jana alishindwa kuamka mapema, hata
hivyo hakuweza kuhisi jambo lolote: “Ilipofika saa 12 asubuhi nikaanza
kusikia watu wakishangaa kitu nje, nilipotoka nikakuta nyungo na
tunguri ndani yake…mara wakaja vijana wawili na pikipiki wakachukua
ule ungo na kukimbia nao…nikawatuma vijana wawafuate waurudishe…
walifanikiwa na nyungo ile ilirejeshwa nyumbani hapa na ndipo
nilipouteketeza kwa moto.

Nilidhani yatakuwa yameisha, lakini wananchi waliendelea kudai
nimewafungia wahuska ndani, si kweli hakuna mtu humu ndani wala mimi
sijui kilichotokea hadi hivyo vitu vikawa humu ndani.”

Katika mapambano hayo ya wananchi na polisi, wananchi kwa kutumia mawe
wamemjeruhi Mwandishi wa Habari wa Channel Ten mkoani hapa, John
Kasembe kwa jiwe kichwani, sehemu za kisogoni ambapo ametibiwa
zahanati ya Fajima na anaendelea vizuri.

Kwa mujibu wa Kasembe, alipigwa mawe kichwani akiwa kazini kukusanya
habari na wananchi waliokuwa wakiwarushia mawe polisi.

Ofisa wa polisi ambaye jina lake hakutaka litajwe kwa sababu si
msemaji wa jeshi hilo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza
kuwa gari moja ya polisi PT 1421 limevunjwa kioo cha mbele kwa mawe.

Hadi saa 10.00 jioni bado polisi walikuwa wanaendelea kupiga mabomu ya
machozi hewani huku wananchi wakionekana kujipanga katika makundi hali
iliyotishia usalama wa maeneo hayo.



Chanzo: Wanabidii Forums

No comments :

Post a Comment