dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, February 13, 2013

CCM JUU YA GESI YA MTWARA!

TAMKO LA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CCM KUHUSU MAANDAMANO NA VURUGU ZILIZOTOKEA MKOANI MTWARA JUU YA UJENZI WA BOMBA LA GESI NA MAENDELEO YA MKOA WA MTWARA


1. Halmashauri Kuu ya Taifa imepokea maelezo ya Serikali kuhusu maandamano na vurugu zilizotokea Mkoani Mtwara tarehe 27 Desemba, 2012 tarehe 25 Januari, 2013 na tarehe 26 Januari, 2013. Maandamano na vurugu hizo zilizodaiwa kuwa na lengo la kupinga mradi wa bomba la Gesi kujengwa na kupeleka Gesi Dar es Salaam.

2. Baada ya kupokea maelezo haya ya Serikali, Halmashauri Kuu ya Taifa imebaini kuwa: -

(a) Kwa sehemu kubwa Wananchi wa Mkoa wa Mtwara hawakuwa wamepewa elimu ya kutosha juu ya uendelezaji wa Gesi na jinsi watakavyonufaika.

(b) Baadhi ya Wanasiasa na baadhi ya Viongozi wa Makundi mbalimbaliwaliamua kutomia suala la Gesi kupandikiza lugha za chuki, uchochezi na upotoshaji wa maendeleo ya Mradi wa Gesi kwa lengo la kujitafutia umaarufu.

(c) Suala la Gesi limetumika kama kisingizio tu cha kufanya vitendo vya rurugu na uvunjifu wa amani.

3. Kutokana na ukweli huu, Halmashauri Kuu ya Taifa inaelekeza ifuatavyo:-

(i) Imesikitishwa na vurugu zilizotokea na kusababisha watu kadhaa kupoteza maisha na uharibifu mkubwa wa mali na majengo ya CCM,Serikali, Wabunge na watu binafsi. Halmashauri Kuu ya Taifa inawapa pole wafiwa na waliopoteza mali zao.

(ii) Inaiagiza Serikali kufanya uchunguzi wa kina kuhusu waliofanya vurugu na uharibifu mbalimbali na kuwachukulia hatua kwa mujibu wa Sheria. Pia, kuwa makini na kuhakikisha matukio kama haya hayajitokezi tena.

(iii) Inaiagiza Serikali kuendelea kutoa elimu ya kutosha kwa Wananchi wamaeneo husika kuhusishwa na kuelimishwa juu ya miradi mbalimbali kwenye maeneo yao.

(iv) Halmashauri Kuu ya Taifa inawataka Wananchi wa Mkoa wa Mtwara kuendelea kuishi kwa amani na utulivu kama ilivyo desturi yao, maana vurugu pamoja na kuharibu mali na kugharimu maisha vinaweza kuwakimbiza wawekezaji waliojitokeza na ambao shughuli zao zitawafaidisha wananchi wa Mkoa huu na Watanzania kwa ujumla .


HALMASHAURI KUU YA TAIFA
Dodoma 10 – 11 Februari, 2013

No comments :

Post a Comment