Written by Ahmed Omar Khamis // 31/05/2013
Source: Mzalendo
Je unayo habari? Je umesahau? ni wazanzibari, wapenda nchi yao, wazalendo, wanaharakati, wana kindakindaki na wale wanaosema kwa yakini ya mioyo yao na kuthibitisha kwa vitendo vyao mapenzi makubwa ya nchi yao. Wale wanaoamini kwamba “vyovyote na iwe lakini Zanzibari ibaki huru yenye mamlaka yake kamili”. Umma huo utakusanyika kesho Jumamosi tarehe 01/06/2013 katika viwanja vya Demokrasia Kibanda Maiti. Uwanja wa Kibanda Maiti utageuka “Tahrir Square” ya Misri na kuudhihirishia ulimwengu kwamba wazanzibari kwa amani kabisa wanataka mamlaka kamili ya nchi yao tukufu. Unamuogopa nani ewe mzanzibari? Ogopa nchi yako kuendelea kuwa chini ya ukoloni. Hapa ni Zanzibar kwanza, itikadi ni baadae. Viongozi mbali mbali wa vyama mbali mbali wazalendo wenye uchungu na nchi yao wanatarajiwa kuhudhuria.
Shime wazanzibari tujitokeze kwa wingi. Mambo yataanza saa 2:00 za asubuhi mpaka saa 12:00 jioni. Mgeni Rasmi ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.
TUNATAKA NCHI YETU SASA TUMECHOKA TAFRANI
ZANZIBAR KWANZA!
TUNAPATIKANA LIVE: http://www.ustream.tv/channel/mazruimedialive
No comments :
Post a Comment