dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, September 26, 2014

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar Yawatunukia Wafanyakazi Bora 2013.

Viongozi wakiwa mgeni rasmin Mkurugenzi wa ZAT Ndg. Marhoon Tobby, wakiimba wimbo wa mshikamano kwa wafanyakazi wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi kwa Wafanyakazi Bora 15 wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar.

Wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar wakijumuiya katika kuimba wimbo maalum wa Wafanyakazi katika sherehe za kutowa zawadi kwa Wafanyakazi Bora.

 Wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar wakijumuiya katika kuimba wimbo maalum wa Wafanyakazi katika sherehe za kutowa zawadi kwa Wafanyakazi Bora.

Msaidizi Viwanja vya Ndege Zanzibar Ndg.Amour Makame, akitowa maelezo kuhusiana na hafla ya sherehe za kutowa zawadi kwa wafanyakazi Bora wa Idara hiyo iliofanyika katika Ofisi za Viwanja vya ndege kisauni Zanzibar.


Mkurugenzi Rasilimali Watu Ndg.Muhidin Tahir, akihutubia na kutowa machache kuhusiana na hafla hiyo ya kukabidhi zawadi kwa wafanyakazi bora kwa mwaka 2013.na kuzungumzia ufanisi wa Wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar katika kazi zao kuwapongeza kwa kuchaguliwa wafanyakazi bora na kuongeza bidii katika majukumu yao ya kila siku kazini.    

Mfanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndegev Zanzibar akisoma risala kwa niaba ya wafanyakazi wa Viwanja vya ndege wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika ofisi zao kiembesamaki Zanzibar, 
Baadhi ya Wafanyakazi na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar wakiwa katika ukumbi wa sherehe za kukabidhiwa Wafanyakazi Bora wa Idara hiyo iliofanyika katika jengo la Ofisi za Mamlaka kiembesamaki Zanzibar. 

Kaimu Katibu Mkuu ZATCU Ndg.Abdalla Ali Vuai, akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa ZATCU, wakati wa sherehe za kuwatunukia Vyeti wafanyakazi Bora wa Mamlaka ya Viwanja vya ndege Zanzibar, jumla ya wafanyakaszi 15 wamepata zawadi na vyeti kutoka Chama cha Wafanyakazi ZATCU.
  
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Viwanja vya Ndege Zanzibar Ndg. Juma Saleh, akiwahutubia Wafanyakazi Bora wa Viwanja vya Ndege Zanzibar wakati wa sherehe za kuwakabidhi zawadi na Vyeti, kwa kuchaguliwa wafanyakazi bora na kuwata kuongeza juhudi katika majukumu yao ya kazi wasiridhike kwa kuchaguliwa wafanyakazi bora wote ni bora lakini wao ni zaidi. 

Baadhi ya Wafanyakazi na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar wakiwa katika ukumbi wa sherehe za kukabidhiwa Wafanyakazi Bora wa Idara hiyo iliofanyika katika jengo la Ofisi za Mamlaka kiembesamaki Zanzibar. 

Mkurugenzi wa Kampuni ya ZAT Ndg. Marhoon Tobby, akizungumza na kutowa nasaha zake kwa Wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar, wakati wa sherehe za kukabidhiwa Vyeti wafanyakazi Bora. kwa mwaka 2013.



MKURUGENZI wa Kampuni ya ZAT Zanzibar Ndg. Marhoon Tobby, akimkabidhi zawadi mmoja wa Mfanyakazi Bora wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar , Bi Nuru Ali Issa, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ofisi hiyo uwanja wa ndege kiembesamaki  jumla ya wafanyakazi bora 15 wamezawadia Vyeti na fedha tasilim.


Mkurugenzi wa Kampuni ya ZAT Zanzibar Ndg. Marhoon Tobby, akimkabidhi zawadi mmoja wa Mfanyakazi Bora wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar.Bw. Mansoor Ahmed Abubakar, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ofisi hiyo uwanja wa ndege kiembesamaki  jumla ya wafanyakazi bora 15 wamezawadia Vyeti na fedha tasilim.

 Mgeni rasmin Mkurugenzi ZAT Ndg.Marhood Toby na Viongozi wa Mamlaka ya viwanja vya Ndege Zanzibar wakiwa katika picha ya pamoja nje ya jengo la VIP uwanja wa ndege Zanzibar.

Wafanyakazi Bora wa Idara ya Mamlaka ya Viwanja vwakiwa katika picha ya pamoja baada kukabidhiwa zawadi na Vyeti vyao kwa kuwa wafanyakazi bora kwa mwaka 2014,wakiwa nje ya jengo la VIP uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume. 
Chanzo: ZanziNews

No comments :

Post a Comment