Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni Zanzibar Mhe.Hamad Yussuf Masauni,
akizungumza na mafundi wa Mamlaka ya Maji Zanzibar wakiwa katika
harakati za kuunga mabomba ya maji kwa ajili ya Mradi Mkubwa wa maji kwa
jimbo la kikwajuni unaokaribia tamati ya mradi huo kqwa kuweka maboimba
hayo tayari kiasi kikubwa yameshawekwa na sasa wanamalizia kilimani
mnara wa mbao kuunganisha katika tangi jipya lililofungwa katika mnara
huu kwa ajili ya kusambaza Maji kwa wananchi wa kikwajuni na jirani zao.
Mbunge wa Kikwajuni na Wananchi wa jimbo hilo wakishiriki katika zoezi
la kuweka mabomba kwa ajili ya kutolea huduma hiyo kupandisha katika
tenki la mnara wa mbao kilimani na kusabazwa kwa wananchi wa jimbo la
kikwajuni na jirani zao.
Mbunge wa Kikwajuni Mhe. Hamad Yussuf Masauni akiwa na mafundi wa ZAWA
wakiunganisha mabomba ya maji kwa ajili ya kumalizia Mradi wa kusambaza
maji safi na salama kwa jimbo lake wakiwa katika maeneio ya kilimani
mnara wa mbao baada ya kutandika bomba kutoka katika kisima kipya
kilichochimbwa kaburi kikombe ili kutowa huduma ya maji kwa Wananchi wa
Kikwajuni, Kilimani na maeneo jirani.
No comments :
Post a Comment