Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alisema kitendo hicho cha wajumbe hao hasa mawaziri ni kitendo kibaya na ni kumdhalilisha rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.
Alisema CCM kimeshangaa na hawakutarajia kitendo hicho kutokea hasa ikizingatiwa kuwa CCM na CUF wamekubaliana na kuunda serikali ya umoja wa kitaifa.
“Kilichotushtua ni mawaziri kutoka CUF kuungana na wajumbe wezao kususia kikao kwa lengo la kukwamisha muswada wa sheria wa kuidhinisha matumizi ya fedha za bajeti na kama mswada huo ungeshindwa kupitishwa serikali ingeshindwa kufanya mambo yake ya msingi,” alisema Vuai.
Aliongeza: ”Kitendo kile sisi tunakiita ni vichekesho na vituko kwani inaonyesha dhahiri yale mapenzi ya CCM kuungana nao na kupatikana kwa SUK ili kuondokana na siasa za chuki na uhasama, wezetu tunaona hawataki hivyo na sisi tutafikiria,” alisema. “Walichokifanya wezetu hawa ni ubakaji wa kidemokrasia na unafiki wa kisiasa kwanini wasitoke mwanzo wa vikao vya bajeti vilipoanza na kuamua kutoka ukingoni ambapo zimebaki siku tatu tu rais kuvunja baraza hilo?” Vuai.
CHANZO: NIPASHE
No comments :
Post a Comment