Muhimbili vitanda vinashushwa na kufungwa leo leo, ni vitanda 500 na magodoro 500.
Kufuatia agizo alilotoa rais Dkt Magufuli kwa Spika wa Bunge kutumia pesa iliyo changwa kwa ajili ya Cocktail party kununua vitanda katika hospitali ya rufaa ya Muhimbili. Agizo hilo limetekelezwa mara moja baada ya vitanda zaidi ya 500 kununuliwa na kuwasilishwa Muhimbili.
Kwa maelezo niliyoyapata kutoka kwa wahusika ni kwamba wanatarajia kununua vitanda vingine zaidi wiki hii na kuvipeleka kwenye hospitali za wilaya ili vikasaidie wagonjwa katika hospitali hizo na kupunguza changamoto ya wagonjwa kulala chini. Picha hizi hapa chini zikionyesha vitanda hivyo vikiwasili katika moja ya kalakana za MSD.
No comments :
Post a Comment