dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, February 23, 2018

Waombolezaji waporwa mabango msiba wa Akwilina!

Baadhi ya waombolezaji ambao walijitokeza kuaga mwili wa marehemu Akwilina aliekua anasoma katika Chuo Cha Usafirishaji (NIT ) jijini Dar es Salaam wamepokonywa mabango mbalimbali ambayo yalikuwa na jumbe mbalimbali kuhusiana na kifo hicho. 
Waombolezaji hao ambao wengine walikuwa wameshika mabango kuhoji uhalali wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Mwigulu Nchemba na IGP Sirro kuendelea kuwepo ofisini mpaka sasa licha ya mauaji hayo kutokea.
Walijitokeza vijana mbalimbali ambao walikuwa wamevaa suti nyeusi na kuanza kupokonya mabango hayo kwa waombolezaji hao na kuondoka nayo, tukio hilo limetokea wakati Waziri wa Elimu, Prof. Ndalichako akihutubia mamia ya waombolezaji katika Viwanja vya Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT).

https://www.eatv.tv/news/current-affairs/waombolezaji-waporwa-mabongo-msiba-waakwilina

No comments :

Post a Comment