Sultan wa mwisho wa Zanzibar aliepinduliwa, Sayyid Jamshid bin Abdallah bin Khalifa, akisalimiana na Mkuu wa Upinzani katika Baraza la Taifa (Bunge) la Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Afro Shirazi Party (ASP), Sheikh Abeid Amani Karume ambaye alikuwa ni mmoja wa viongozi waliokwenda bandarini Unguja kumlaki Sultan huyo akitokea kisiwani Pemba alikofanya ziara mwezi Desemba 1963 ikiwa ni mwendelezo wa Sherehe za Uhuru wa Zanzibar. Ziara hio ilikuwa ni ya mwisho, kwani mwezi mmoja baadae Sultani alipinduliwa.
Hili blog ni kuhusu Tanzania na dunia nzima kwa ujumla. Pita kila siku kwa habari moto moto. (This blog is about Tanzania and the world as a whole. Pass-by everyday for breaking news). ***********************KARIBUNI NYOTE / YOU ARE ALL WELCOME!***********************
No comments :
Post a Comment