“Kama Polepole anataka kutoka atoke atuachie CCM maana ana wenzake wanaomshawishi kuanzisha chama chao, asitapetape na kuongea mambo ambayo hayaeleweki.”
"Hawa kina Polepole waliojificha hawatusumbui ndani ya CCM kwa mujibu wa kanuni na katiba ya chama kama mwanachama anaenda tofauti kuna onyo, kufungiwa au kufukuzwa uanachama.”
Bulembo amesema anamfahamu Polepole tangu mwaka 2012 alipoteuliwa na rais mstaafu Jakaya Kikwete kuwa mjumbe wa iliyokuwa tume ya mabadiliko ya katiba.
"Siyo kwamba ndani ya CCM tulifurahia uteuzi wake wa ukatibu mwenezi Taifa bali tuliheshimu mamlaka ya aliyekuwa mwenyekiti Taifa hayati John Magufuli bali. Hamjali Samia na kimsingi hawezi kumpangia rais cha kufanya, yeye ni nani,”amesema Bulembo.
#edwinmoshiupdates
Chanzo: Mwananchi
No comments :
Post a Comment