dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, December 12, 2021

MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA UHURU WA NCHI ILIYOKUWA IKIITWA TANGANYIKA (TANZANIA BARA) KATIKA JIJI LA WASHINGTON, DC!

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe, Elsie Kanza akiongea jambo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mhe. Peter Lord anayeshughulikia naswala ya Afrika Mashariki, Sudan na Sudan ya Kusini siku ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara siku ya Alhamisi Disemba 9, 2021 katika Hotel ya Washington, Marriott iliyopo Washington, DC, 
Picha juu na chini ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe, Elsie Kanza akisoma hotuba yake kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara siku ya Alhamisi Disemba 9, 2021 katika Hotel ya Washington, Marriott iliyopo Washington, DC,, Katiba hotuba hiyo, Mhe, Balozi alielezea historia ya Tanzania Bara miaka ya 60 na mashirikiano ya Tanzania na Marekani ikiwemo Mexico, Mashirikiano ya Tanzania Bara wakati huo ikiitwa Tanganyika yalianzia tangu enzi ya Mwalimu Nyerere na Rais wa Marekani wakati huo hayati John F, Kennedy.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe, Elsie Kanza akipongezwa kwa hotuba nzuri na Balozi wa Rwanda Mhe. Mathilde Mukantabana.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mhe. Peter Lord anayeshughulikia naswala ya Afrika Mashariki, Sudan na Sudan ya Kusini akisoma hotuba yake akipongeza mashirikiano katika nyanjambalimbali kati ya Marekani na Tanzania na kuipongeza Tanzania kuadhimisha maiaka 60 ya Uhuru.
Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Elsie Kanza akimshukuru Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mhe. Peter Lord anayeshughulikia naswala ya Afrika Mashariki, Sudan na Sudan ya Kusini kwa hotuba yake,
Picha juu na chini Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe, Elsie Kanza akisamilia na kubadilishana mawili, matatu na wageni mbalimbali wakiwemo waheshimiwa Mabalozi na Waambata wa Jeshi wa Balozi zao.
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi

Picha juu na chini Mabalozi kutoka nchi mbalimbali, Wambata wa Jeshi kutoka Balozi zao na wageni waalikwa wakiwasili wengine wakiendelea na mchapalo wa maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara uliofanyika siku ya Alhamisi Disemba 9, 2021 katika hotel ya Washington, Marriott, Washington, DC
Mshereheshaji Tuma akisherehesha maadhimisho hayo.
Nyimbo za Taifa Marekani na Tanzania zikipigwa kuashiria ufunguzi rasmi wa maadhimisho hayo ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
Picha juu na chini Mabalozi kutoka nchi mbalimbali, Wambata wa Jeshi kutoka Balozi zao na wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya Mhe. Balozi wa Tanzania nchini Marekani alipotoa hutuba siku ya maadhimisho ya miaka 60 6a Uhuru wa Tanzania Bara,

Msanii wa kikundi cha Tanzanite African Acrobatics kutoka Miami akiwatambulisha wasanii wenzake kwenye kundi hilo walipokua sehemu ya kusherehesha maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara uliofanyika siku ya Alhamisi Disemba 9, 2021 katika hotel ya Washington, Marriott, Washington, DC. Kundi lina wasanii wanne Matiga Kobs, Emmanuel Mbonde, Faraji Ngingite na Sadick Shabani
Juu na chini kikundi hicho kikisherehesha siku ya maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara,
Mshereheshaji Tuma
Wasanii wakiwa katika picha ya pampja,
Juu na chini ni picha za pamoja na Balozi

No comments :

Post a Comment