dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, December 10, 2021

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI CANADA WASHEREHEKEA MIAKA 60 YA UHURU WA ILIYOKUWA IKIITWA TANGANYIKA!

Ubalozi wa Tanzania nchini Canada ambao upo jijini Ottawa jana jioni ulisherehekea miaka 60 ya Uhuru wa nchi ambayo iliyokuwa ikiitwa Tanganyika ambayo katika mwaka 1964 iliungana na JAMHURI YA WATU WA ZANZIBAR na kuunda JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na Wa-Tanzania kadhaa kutoka sehemu mbali mbali za Canada na pia zilihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Canada H.E. Dr. Mpoki Ulisubisya.

Sherehe hizo za Uhuru zilifanyika nje kidogo ya jiji la Toronto kwenye hoteli maarufu ijulikanayo kama Hilton Garden Inn, Toronto Airport, kwenye Drive ya Caroga #3311, Mississauga, Ontario.

Habari muhimu iliyosambazwa katika sherehe hizo ni kuwa Balozi atakuwa na mkutano wa zoom tarehe 11 December saa 11 za jioni (Eastern) na topic itakuwa: TANZANIAN DIASPORA IN CANADA REFLECTING ON THE PAST 60 YEARS  pamoja na kujibu masuala ya Wana-Diaspora.
Anaepewa mkono ni H.E. Dr. Mpoki Ulisubisya - High Commissioner wa Tanzania nchini Canada, kulia yake ni Board Member wa Jumuiya ya ZACADIA (Zanzibar-Canadian Diaspora Association) Nd. Hemed Zahor.


Support us by considering joining our Patreon scheme at: 
BECOME A PATRON TODAY!


No comments :

Post a Comment