dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, September 26, 2017

Myweather anunua jumba la bilioni 56!

 KWA watu wengi, kumiliki majumba Las Vegas na Miami ingetosha kuwafanya waone wameshamaliza kazi, lakini Floyd Mayweather yupo tofauti na wengi.

Bondia huyo Mmarekani ambaye hajawahi kupigwa katika pambano lolote kati ya mapambano yake 50 aliyocheza, anaendelea ku­furahia maisha ya kustaafu baada ya kumchapa Muiri­shi, Conor McGregor jijini Las Vegas.

Baada ya kumchapa McGregor katika raundi ya 10, inadaiwa Mayweather aliweka kibindoni zaidi ya pauni milioni 250 (Sh bil­ioni 752).

Bondia huyo ambaye amekuwa hajivungi ka­tika matumizi ya fedha na kufurahia jasho lake, amemwaga kitita cha pau­ni milioni 18.9 (zaidi ya Sh bilioni 56) kununua jumba kubwa la kifahari, katika eneo la watu wazito la Beverly Hills.Kumbuka kuwa, Mayweather, 40, ana jumba jingine jijini Las Vegas, pia analo jingine Miami ambalo lina thamani ya pauni milioni 5.69 (zaidi ya Sh bilioni 17).

Jumba hili jipya alilonunua, lina vyumba sita vya kulala na mabafu kumi. Pia lina chumba maalu­mu cha sinema ambacho wanaweza kukaa watu 50 kwa raha kabisa, likiwa na mbwembwe nyingi zikiwemo mvinyo, bisi, chocolate na pipi.

Mayweather amecheza ngumi kwa miaka 21 na alistaafu Agosti 26 akiwa ameingiza fedha nyingi zaidi ya bondia yeyote yule kihistoria

Mmarekani huyo anadai kuwa yeye ndiye bondia wa kwanza kuingiza zaidi ya dola bilioni moja (zaidi ya Sh trilioni 2) katika mchezo huo mgumu zaidi.

Ukiachana na mkwanja aliotumia katika ku­nunua jumba hilo, inasemekana pia kuwa May­weather ametumia kiasi cha pauni 369,000 (zaidi ya Sh bilioni moja) kwa ajili ya kununua vitu vya ndani.













No comments :

Post a Comment