dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Tuesday, November 28, 2017

Makamu wa rais Samia Suluhu amtembelea Lissu hospitali!


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu Hassan, amekwenda hospitali kumuona mbunge wa Singida Mashariki Tundu Antiphas Lissu, ambaye amelazwa kutokana na kupigwa risasi.

Mama Samia ambaye alikuwa jijini Nairobi kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, aliwasili hospitalini hapo jioni hii akiwa ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Kenya Dkt. Pindi Chana.

Makamu wa Rais mama Samia Suluhu anakuwa kiongozi wa kwanza mkubwa kitaifa kwenda kumuona mbunge huyo ambaye yupo hospitalini hapo tangu Septemba 7 alipopigwa risasi na watu ambao hawajajulikana mpaka sasa.

No comments :

Post a Comment