dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, August 31, 2018

" Mwalimu atakaevunja sheria atapata viboko" RC Kagera!

Katika kuhakikisha kitendo kilichotokea mkoani Kagera cha mwanafunzi kupigwa na kusababishiwa kifo hakitokei mkoani Tanga, mkuu wa mkoa huo Martine Shigela amewaagiza viongozi wa mkoa huo kusimamia sheria za adhabu mashuleni.

Akiongea leo kwenye kikao cha robo ya tatu ya mwaka cha kamati ya ushauri ya mkoa (RCC), Shigela amesema mwalimu atakayebainika kutoa adhabu kinyume na utaratibu naye aweze kuadhibiwa kama ilivyokuwa kwa mwanafunzi.

''Mwalimu akienda kinyume na sheria ya adhabu mashuleni maana yake kajitengenezea sheria yake ambayo haijatungwa na bunge hivyo kwa kosa hilo lazima iwepo adhabu kwa mwalimu aliyevunja sheria na kwasababu anakuwa ametoa adhabu ya viboko ni vyema na yeye akapata viboko kama alivyo mchapa mwanafunzi'', amesema.

Kwa upande wake afisa elimu mkoa wa Tanga Mayasa Hashim amewaasa walimu kufuata utaratibu wa aina ya adhabu anazopaswa kupewa mwanafunzi huku akiongeza kuwa sio kila kosa linahitaji adhabu bali makosa mengine yanatakiwa kuishiwa kwa mwalimu kumshauri mtoto ili asirudie.

No comments :

Post a Comment