dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, August 23, 2019

Zanzibar kununua Mtambo mpya wa uchapaji Magazeti!


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein emesema kuwa dhamira ya Serikali ya kununua Mtambo mpya wa uchapaji wa magazeti ni kuhakikisha kiwango cha uchapishaji wa magazeti ya Zanzibar leo kinaongezeka.

Dk. Shein amesema hayo Ikulu mjini Zanzibar, wakati akipokea taarifa ya Utekelezaji wa Mpango Kazi kwa Wizara Habari, Utalii na Mambo ya Kale kwa kipindi cha Julai 2018 – Juni 2019.

Amesema hatua ya Shirika la Magazeti ya Serikali kuchapisha nakala 1,500 katika mtambo ya ZAGPA kwa siku ni kidogo mno ikilinganishwa na uwezo mkubwa wa mtambo huo wa kuchapisha nakala 35,000 kwa saa moja.
Alisema kuwepo kwa mtambo huo kunapaswa kwenda sambamba na kiwango kikubwa cha uchapishaji wa magazeti ili yaweze kuwafikia wananchi hadi walioko mjini na vijijini.

Aidha, alisema kuna umuhimu wa kuwa na Mawakala wa uuzaji na usambazaji wa magazeti Mikoani, watakaokuwa na jukumu la kupokea magazeti hayo na kuyasambaza katika shehia mbali mbali na kuwafikia wananchi.

Katika hatua nyengine, Dk. Shein alieleza haja kwa baadhi ya vyombo vya habari nchini kutumia vyema lugha ya Kiswahili, katika utangazaji na uandishi wa habari akibainisha hali halisi kuwa Zanzibar Mjini ndio kitovu cha lugha fasaha ya Kiswahili.


Hivyo alitumia fursa hiyo kuuagiza uongozi wa Wizara hiyo kukutana na wahariri wa vyombo vya habari, kwa lengo la kuipatia ufumbuzi changamoto hiyo.

Aidha, aliitaka Idara ya Habari Maelezo Zanzibar, kuweka utaratibu mzuri wa kutoa Vibali vya kupiga picha, na kusisitiza umuhimu wa kufuatwa sheria za nchi, hasa kwa wageni wanaokuja kufanya shughuli hizo hapa Zanzibar.

Aidha, Dk. Shein alisisitiza haja ya kuendelea kuzitunza na kuzihifadhi vyema nyaraka za Serikali.

Dk. Shein alisisitiza haja kwa uongozi wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma kuharakisha utekelezaji wa uamuzi wa serikali wa kuanza maandalizi ya msingi ili kukiwezesha Chuo hicho kuunganishwa na Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA).

Akigusia uendeshaji wa shughuli za makumbusho, Dk. Shein aliitaka Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale, kuendelea kuishajiisha jamii ya Wazanzibari, ikiwemo wanafunzi, kutembelea maeneo hayo ili kufahamu historia ya asili ya Zanzibar.

Aidha, Rais Dk. Shein alisiitiza haja ya kuendeleza uhusiano na ushirikiano mwema uliopo katika sekta ya Utalii, kati ya Zanzibar na Indonesia kwa kushirikiana na Chuo cha Utalii cha Bali cha nchini Indonesia.

Dk. Shein aliupongeza uongozi wa Wizara hiyo kwa kutekeza vyema majukumu ya kazi zake, sambamba na kuandaa kwa umakini mkubwa tarifa za Utekelezaji wa mpango kazi.

Nae, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, alisisitiza umuhimu wa watendaji an wafanyakazi wa Serikali kufanya kazi kwa uadilifu na kutoa pongezi kwa Wizara hiyo kwa mafanikio iliyoyapata sambamba na kuwasilisha vyema mpango kazi wake.

Mapema, Waziri wa Wizara hiyo, Mahamoud Thabit Kombo alisema katika kipindi cha Julai – Juni 2018/2019 Wizara imefanikiwa kutekeleza miradi mikuu mitatu, ukiwemo wa ujenzi wa Studio na Ofisi za ZBC Pemba, kupitia Kampuni ya ujenzi ya Chuo cha Mafunzo Zanzibar, ambapo awamu ya kwanza ya kazi hiyo inayohusisha ghorofa ya chini imekamilika.

Alisema awamu ya pili ya ujenzi huo, Mkandarasi ataendelea na kazi itakayohusisha ujenzi wa ghorofa ya pili, uwezekaji, upigaji wa palasta pamoja upakaji wa rangi.

Aidha, alisema katika kipindi hicho, Wizara ilishughulikia mradi wa kuimarisha maeneo ya kihistoria ya Fukuchani na Makamandume, mradi ulioogharimu shilingi Milioni 850.

Alisema Wizara imeweza kulifanyia matenegenzo makubwa eneo la kihistoria la Fukuchani, ili kurudisha sura na haiba yake ya awali.

Alisema matengenezo ya eneo la kihistoria la Mkamandume yanaendeleo, ukilenga kuziimarisha kuta za asili katika pande tatu za jengo hilo pamoja na kuvirudisha baadhi ya vivutio vya asili vilivyomo ndani ya eneo hilo.

Vile vile, alisema katika kipindi hicho Wizara ilishughulikia mradi wa kuimarisha Utalii kwa wote, ukihusisha ujenzi wa kituo cha Utalii katika eneo la Kwa Bihole Bungi, mradi utakaotumia shilingi Bilioni 1.3 hadi kukamilika kwake.

Alisema hatua ya kwanza ya ujenzi zimeanza chini ya Mkanadarasi Quality Building Contarctor, na kubainisha kuwa pale utakapomalizika utaongeza vivutio vya utalii nchini, kuimarisha utalii wa ndani na kimataifa, pamoja na kuongeza ajira kwa jamii, hasa vijana.

Wakati huo huo, Dk. Shein alikutana na uongozi wa Wizara ya Katiba na Sheria na kuipongeza kwa utekelezaji mwema wa majukumu ya kazi sambamba na uwasilishaji mzuri wa taarifa ya mpango kazi.

Dk. Shein alitumia fursa hiyo kuishauri Wizara hiyo kuzingatia haja ya kuwa na utaratibu maalum katika utengenezaji wa sheria mpya, ili kuwepo mustakbali mwema wakati ssheria hiyo itakapohitaji kufanyiwa marekebisho au kufutwa kabisa.

Nae, akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya Mpango kazi kwa kipindi cha Julai 2018 – Juni 2019, Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria Khamis Juma Mwalimu alisema pamoja na mambo mengine Wizara imefanikiwa kuimarisha mfumo wa sheria kwa kufanya mabadiliko ya utendaji kazi wa mahakama,Ofisi ya DPP, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Polisi, Mafunzo na wadau wengine wa sheria ili kuwajengea uwezo katika utoaji haki.

Alisema katika utekelezaji wa majukumu yake, Wizara ilikabiliwa na changamoto ya uhaba wa watendaji hasa baada kuigaiwa kwa iliokuwa Ofisi ya Rais, Katiba,Sheria na Utumishi wa Umma na Utawala bora, pamoja na kuanzishwa kwa Idara mpya ya msaada wa kisheria.

Aidha, alisema katika kulipatia ufumbuzi suala hilo, Wizara inakusudia kuajiri watendaji kutoka katika Kada tofauti ili kukidhi mahitaji ya Wizara.


No comments :

Post a Comment