Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, leo imetangaza rasmi maombi ya kila anaetaka kuwekeza mji mkongwe. Apeleke maombi yake sio zaidi ya tarehe 9/7/2021. Fomu zipo mji mkongwe afisi ya uhusiano. Au aingie www.utaliismz.go.tz.... ipo link ya fomu ajaze na awasilishe maombi yake ndani ya muda ulopangwa.
Majibu yatatolewa ndani ya wiki baada ya muda wa maombi kumalizika.
Masharti ya maombi:
1. Muombaji apendekeze atalipa kiasi gani kwa serikali (uplift).
2. Aeleze aina na lengo la uwekezaji wake.
3. Awe tayari kufuata ushauri wa utaalam wa mji mkongwe wakati wa ujenzi
4. Aeleze jinsi ambavo atalitengeneza jengo.
5. Kodi itapangwa kulingana na gharama alizotumia katika ujenzi.
Shukran.
No comments :
Post a Comment