dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Friday, October 26, 2012

DR SHEIN ATOA ONYO KALI KWA WANAOVURUGA AMANI YA ZANZIBAR.

Dk. Ali Mohamed Shein 

Written by   //  26/10/2012

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa ustahamilivu na uvumilivu wa Serikali umefikia kikomo kwa wale wote wanaofanya vitendo vya fujo na vurugu na itamshughulikia ipasavyo mtu yo yote atakaevunja sheria.
Dk. Shein aliyasema hayo leo katika hotuba yake aliyoitoa kwenye Baraza la Idd el Hajj
Lililofanyika huko katika hoteli ya Bwawani mjini Zanzibar.
Katika hotuba yake hiyo Dk. Shein alisema kuwa ustahamilivu na utulivu sio udhaifu ni heshima kubwa ya kutii amri ya MwenyeziMungu na kusisitiza kuwa hatua ya serikali kuvumilia vitendo hivyo vya uvunjifu wa amani sasa basi. “enough is enough”, alisisitiza Dk. Shein.
Dk. Shein alieleza kuwa Serikali itafanya kila inavyowezekana ili kuhakikisha kwamba wanaohatarisha usalama na amani hapa ncdhini wanachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria zilizopo.
Alisema kuwa Serikali itatumia sheria na taratibu zilizopo ili kuvishughulikia vitendo vya uvunjifu wa wa amani vitakavyofanywa au kuchochewa na kikundi chochote na kusisitiza kuwa hakuna hata mtu mmoja alie juu ya sheria bali kila mtu anapaswa kufuata sheria.
Dk. Shein alieleza kuwa hatua za kisheria tayari zimeshaanza kuchukuliwa na tayari viongozi wanane wa Jumuiya ya UWAMSHO wamepelekewa mahakamani na wengine waliokamatw3a na polisi kwa kufanya fujo nao pia wameshafikishwa mahakamani.
Alisema kuwa wakati huo huo Jeshi la Polisi na vyombo vya Ulinzi na Usalama vitaendelea na doria katika mitaa mbali mbali ili kuhakikisha kuwa wananchi wanaishi kwa amanhi na kueleza kuwa mali za watu na maisha yao yataendelea kulindwa.
Alieleza kuwa fujo zilizotokea Oktoba 17 mwaka huu, zilipelekea kuchomwa kwa maskani za CCM, kuvunjwa maduka, kuporwa kwa mali za watu na kuharibu miundombinu ya barabara na uharibifu mwengineo.
Vile vile Dk. Shein alieleza kuwa fujo na vurugu hizo zilipelekea kuuliwa kwa askari wa Polisi wa kikosi cha FFU Namba F2105, Koplo Said Abdulrahman na kutoa pole kwa wafiwa, ndugu na jamaa wa marehemu.
Alisema kuwa kiini cha fujo hizo inasadikiwa kuwa ni wafuasi wa Sheikh Farid Hadi, kiongozi wa UWAMSHO, waliodai kuwa Sheikh wao huyo haonekani na hivyo kudhania kuwa anashikiliwa na vyombo vya dola, madai ambayo hayakuwa ya kweli;
“Jeshi letu la Polisi na vyombo vya Ulinzi na Usalama viko imara katika kuvidhibiti vitendo vya fujo na vurugu… napenda kukuhakikishieni wananchi nyote kwamba Serikali itaendelea kuchukua hatua madhubuti dhidi ya watakaotishia amani ya nchi yetu”,alieleza Dk. Shein.
Aidha, Dk. Shein aliwanasihi wananchi wote kuimarisha umoja na mshikamano ambao ndio msingi mkubwa wa amani na utulivu uliopo na kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaosababbisha uharibifu na kuitia hasara Serikali.
Pamoja na hayo, Dk. Shein alisema kwua Serikali itajitahidi kuzifanyia kazi changamoto zote zilizo ndani ya uwezo wake ili kuwasideia wakulima na kuelekea katika lengo kuu la Serikali la kuimarisha sekta ya kilimo kwa lengo la kuyafanikiwa Mapinduzi ya Kilimo.
Alitoa wito kwa wakulima na wananchi kuzitumia mvua za Vuli pale zitakaponyesha kwa ajili ya kilimo na pia, kwa ajili ya upandaji wa miti ya misitu, biashara na matunda.
Alisisitiza pia wananchi wafuate taratibu na sheria za vitendo vinavyosababisha uharibifu wa mazingira na kuzingatia ushauri wa kitaalamu ili mazingira yawe endelevu kama ni njia moja ya kubainisha imani kwa kuwafikiria wengine.
Alieleza kuwa katika kukamilisha sherehe ya Idd hiyo huwa kunahimizwa kuchinja na kuwapa haki waliowajibishwa wakiwemo masikini na marafiki suna ambayo ni kiashirio cha utii alioonesha Nabii Ibrahim.
Alieleza kwua Zanzibar imepiga hatua ya kupigiwa mfano katika maendeleo kwenye nyanja za uchumi na ustawi wa jamii tangu Mapinduzi ya Zanzibar ya tarehe 12 Januari, 1964. Pia alieleza kuwa ripoti ya mapitio ya Dira 2020 iliyotolewa hivi karibuni inaonesha kwamba yapo mafanikio makubwa yaliopatikana.
Mapema asubuhi Dk. Shein aliungana na waumini wengine wa dini ya Kiislamu katika sala ya Idd el Hajj iliyosaliwa katika Msikiti Mushawar, Mwembeshauri na baada ya hapo alikutana na Mashehe na viongozi mbali mbali huko Ikulu waliokwenda kumpa mkono wa Idd.

Chanzo: Mzalendo

No comments :

Post a Comment