Kwarara Msikitini

Dual Citizenship #2

Dual Citizenship #2

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

Mwanakwerekwe shops ad

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Sunday, October 14, 2012

KATIKA KUMUENZI MWALIMU!

*LEO TUNAMKUMBUKA"

The Late President of Tanzania - Mwalimu Julius Nyerere

Uko wapi baba, mwanao mimi nakutafuta/
Ni miaka imepita enzi za baiskeli mpaka sasa kuna Guta/
Njoo upesi baba uwaone wezi wanatupa suluba kimyakimya bila vita/
Ningekutajia majina sema tu moyo unasita.
Wale uliowaacha vijana sasa ni wazee mfano Samweli Sita.
Wale wabunge wako watiifu hawapo tena sasa kuna mafisadi/
Wanataifisha ardhi yako tena hasahasa migodi/
Kisha wanapewa heshma kwa kuchongewa jembe la Gold/
Tuliyemtegemea mtafanana kumbe naye goigoi/
Amekufanana jina tu ila kimatendo bora Toi/
Njoo maramoja baba uturejeshe kwa wakoloni/
Hapa kwenye uhuru tunaishi kama motoni/

Sera ya kujuana inawatesa wanazuoni/
Hata waliosoma sana ajira hivi sasa hawazioni/
Yule mwenye kitambi alituletea shule za kata/
Mwenzake amekuja hana jipya ujinga mtupu amepakata/
Heri tumpe faida mchuuzi tuvujishe hili pakacha/
Hawa wapinzani na watawala nao wanafanana kama mapacha/
Bunge lako tukufu sasa wanaimba kwasakwasa/
Wanapeana mipasho waziwazi wanadai hizo ni siasa/
Sheria zimebadilika sasa askari ruksa kufanya mauaji/
Thubutu kuwakemea nawe uende na maji/
Mgambo wa jiji kamgeuza machinga mtaji/
Ushoga na uchangudoa biashara halali katikati ya jiji/


*LEO TUNAMKUMBUKA"

(Mtunzi hajulikanwi)


No comments :

Post a Comment