dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, October 20, 2012

Raia akiuawa kwanini Rais hatoi rambirambi?

                      JK atoa Pole

20/10/2012 
Rais Jakaya Kikwete, amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema kuomboleza kifo cha askari polisi Said Abdulrahman aliyuawa kikatili visiwani Zanzibar.
Abdulrahman wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), aliuawa kinyama kwa kupigwa mapanga kichwani na mikononi usiku wa Jumatano wiki hii katika eneo la Bububu wakati akirejea nyumbani baada ya kazi kazi.
“Nimesikitishwa na kuhuzunishwa na taarifa za kuuawa kikatili kwa askari wetu Said Abdulrahman wa kikosi cha Kutuliza Ghasia usiku wa tarehe 17 Oktoba wakati akirejea nyumbani kwake, baada ya kukamilisha zamu yake ya kulinda usalama wa raia na mali zao kwa siku hiyo,” alisema Rais Kikwete.
“Kitendo hiki cha mauaji ni kitendo kiovu, ni cha kikatili na kinachostahili kulaaniwa na kufanyiwa kila aina ya uchunguzi ili kuwabaini waliohusika na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria haraka iwezekanavyo,” alisema Rais Kikwete katika salamu hizo.
Alisema anaungana na familia hiyo kumwomba Mwenyezi Mungu, ailaze roho yake mahala pema peponi .

CHANZO: NIPASHE

No comments :

Post a Comment