dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Wednesday, October 24, 2012

SPIKA MAKINDA CANADA!

Spika Makinda ashiriki Mkutano wa 127 wa IPU, Mjini Quebec, Canada. Akutana na Spika wa Morocco

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akisalimiana na mratibu wa 
mahusiano baina ya Global Fund na Mabunge Duniani 
Ndg. Svend Robinson, walipokutana kabla ya kuanza kwa mkutano 
wa 127 wa Chama cha Mabunge Duniani (IPU) unaofanyika 
Mjini Quebec, Canada.

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimtambulisha Mbunge wa 
Bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania Mhe. Dr. Perpetua 
Nderakindo Kessy kwa Balozi wa Tanzania Chini Canada 
Mhe. Alex Massinda kabla ya kuanza kwa mkutano wa 127 
wa Chama cha Mabunge Duniani (IPU) unaofanyika 
Mjini Quebec, Canada.

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akifuatilia taarifa mbalimbali 
na maazimio ya Mkutano wa Chama cha Mabunge Duniani (IPU) 
wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 127 wa IPU Mjin Quebec, Canada. 
Kushoto kwake ni Balozi wa Tanzania Chini Canada 
Mhe. Alex Massinda na Mhe. Hamad Rashid Mohamed.

Mkurugenzi wa Maktaba na Utafiti wa Bunge Ndg. Kileo Nyambele 
anaye muwakilisha katibu wa Bunge Dkt. Thomas kashilila akishiliki 
kikao cha makatibu wa Mabunge yote wanachama wa Mabunge ya 
Dunia (IPU) katika Mkutano wa 127 wa chama hicho mjini Quebec, 
Canada. Kulia kwake ni Afisa dawati la IPU kutoka Tanzania 
Ndg. James Warbarg.

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiongoza ujumbe wa 
Tanzania kupiga kura kuingiza agenda mojawapo kati ya 
agenda 5 za dharura zilizowasilishwa kwa udharura katika 
mkutano wa 127 wa Chama cha Mabunge Duniani (IPU) ili 
zijadiliwe pia. Tanzania iliungana na nchi za Afrika kupigia 
kura agenda ya kujadili hali ya usalama katika nchi ya Mali 
amoja na agenda iliyowasilishwa na Uingereza kujadili kwa 
udharura swala la hatma ya Usalama na Misaada wa Kibinadamu 
Nchini Syria na nchi Jirani. Kushoto kwake ni Balozi wa Tanzania 
Chini Canada Mhe. Alex C. Massinda na Mhe. Hamad Rashid Mohamed.

Spika wa Bunge akitoka katika ukumbi wa Mikutano mara baada 
ya kumalizika kwa kikao cha kwanza katika Mkutano wa 127 wa 
Chama cha Mabunge Duniani (IPU) mjini Quebec, Canada. 
Kushoto kwake ni Mhe. David Kafulila anayehudhuria Mkutano huo pia.

Mhe. Anne Makinda akitoka katika Mkutano na Spika wa Bunge la 
Morocco Mhe. Karim Ghellab kwa lengo la kufanya nae mazungumzo 
ya faragha kuimarisha uhusiano baina ya mabunge ya Tanzania na Morroco.

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akisisitiza jambo wakati 
alipokutana na Spika wa Bunge la Morocco Mhe Karim Ghellab 
kujadili namna bora ya kuimarisha mahusiano baina ya mabunge 
ya nchi zao. Tanzania ilipeleka ujumbe wa Wabunge kutoka kamati 
ya Mambo ya Nje, ulinzi na Usalama kutembelea Bunge la Morocco 
Aprili mwaka huu ikiwa ni sehemu ya kuimarisha mahusiano baina 
ya nchi hizi mbili.

Spika wa Bunge la Morocco Mhe Karim Ghellab akimkabidhi 
Mhe. Spika zawadi mara baada ya kufanya nae Mazungumzo.

Ujumbe kutoka Bunge la Tanzania katika Mkutano wa 127 wa IPU 
Mhe. Hamad Rashid na Mhe. Suzan Lyimo wakifuatilia kwa makini 
mada kuhusu “Multilateralism and the role of parliament in 
parliamentary diplomacy” wakati wa mkutano huo 
Mjini Quebec, Canada.

Chanzo: Vijimambo

No comments :

Post a Comment