dual citizenship

Pemba Paradise

Zanzibar Diaspora

Mwanakwerekwe shops ad

ZanzibarNiKwetuStoreBanner

ZNK Patreon

Scrolling news

************ KARIBUNI..................Contact us for any breaking news or for any information at: znzkwetu@gmail.com. You can also fax us at: 1.801.289.7713......................KARIBUNI

Saturday, October 20, 2012

VURUGU ZANZIBAR!

VURUGU zimeendelea Zanzibar Ijumaa
Written by   //  20/10/2012 
IMG_4213
VURUGU zimeendelea Zanzibar huku mtu mmoja akiuawa baada ya kupigwa risasi ya moto na askari wa Kikosi cha Valantia (KVZ) usiku wa kuamikia jana.
Habari za kuaminika zinasema mtu huyo, Salum Hassan Muhoja mwenye umri wa miaka 30 mkazi wa Regeza Mwendo nje kidogo ya mji wa Zanzibar alipigwa risasi karibu na Amaan mjini hapa.
Inaaminika kuwa mtu huyo alipigwa risasi wakati akipita karibu na baa na nyumba ya kualala wageni Mbawala Amaan ambayo ilivunjwa katika ghasia hizo.
Kijana huyo alitarajiwa kuzikwa jana jioni kijijini kwao Mwera Regeza Mwendo wilaya ya Magharibi Unguja.
Wakati kukiwa na habari hizo za mauaji vijana kadhaa wenye umri wa kati ya miaka 14 na 18 waliingia barabarani eneo la Darajani na kupambana na askari ambao walikuwa wametanda wakilinda doria.
Chanzo: Mzalendo

No comments :

Post a Comment